Matonya - Homa Ya Jiji[NEW AUDIO]@paulmkale

Pakua hapa ngoma mpya ya Matonya"HOMA YA JIJI"Bofya hapo chini kudownload

New Video:Pasha - Mahaba Niue(Official Music Video)

Pasha anakuletea video yake mpya iitwayo"MAHABA NIUE"Ninafasi yako kubonyeza hapo na kuitazama video hii


New Video:Davido ft Uhuru & Dj Buckz - The Sound(Official Music Video)

Staa wa Nigeria David Adedeji Adeleke aka Davido ana hit nyingi tunazozijua Skelewu, Aye na ile Tchelete aliyofanya na wakali wa Mafikizolo, zote ni kali !

Karibu tena mtu wa nguvu fan wa Davido, amekuletea video ya single mpya inayoitwa ‘The Sound’ akiwa amewashirikisha Dj Buckz pamoja na kundi la Uhuru kutoka Afrika Kusini.

Iko hapa, bonyeza play kuenjoy hii #TheSound


Kanye West ft Paul MacCartney - Only one(Official Music Video)

Rapa Kanye West  ameamua kumpa shavu mtoto wake North West katika video mpya ya ‘Only one‘ aliyomshirikisha Paul MacCartney.

Young Killer na hii mipango yake mwaka huu 2015…

Tumeona baadhi ya wasanii ambao bado wapo kwenye masomo lakini wakifanya kazi zao za muziki akiwemo, Stereo, M Rap Lion, Ben Pol, Nikki wa Pili na wengineo, sasa goodnews ninayokusogezea ni hii kutoka kwa mkali wa Hiphop kutoka ROCK CITY Mwanza, Young Killer ambaye kwa mwaka 2015 amesema  atajikita zaidi katika masomo yake.Nadhani utakuwa ni mwaka mzuri pia wa kuendeleza masomo yangu kwasababu mwaka jana niliwahidi watu  na nirudi kweli ila kuna vitu kidogo viliingiliana ikabidi ni stop ila mwaka huu nina plan za kurudi shule.

Nadhani inaweza ikawa mwezi wa tano inshallah mwenyezi mungu akibariki kwa sasa hivi najaribu kuweka mipango sawa, sababu zilizopelekea ni mambo ya kazi zangu yalikuwa yanaingiliana… nikafanya kazi nikusanye pesa ili niweze kujisomesha, mwaka huu kazi nitakuwa nafanya ila nitabase sana kwenye masomo zaidi”Young Killer.

ALI KIBA (@OfficialAliKiba) kupiga shoo ya ‘LIVE’ Sauti za Busara Feb 12 mwaka huu

DSC_0313

Mwenyekiti wa Bodi wa Busara Promotions, wandaaji wa tamasha la Sauti za Busara, Simai Mohammed (katikati) akiongea na wandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati wa mkutano wa wanahabari Jijini Dar es Salaam, juu ya tamasha la 12 la Sauti za Busara, litakalofanyika, Februari 12 hadi 15, mwaka huu, Ngome Kongwe, Zanzibar. Wengine (kushoto) ni Meneja wa tamasha hilo, Journey Ramadhani. na upande wa kulia ni Mkurugenzi wa tamasha hilo, Yusuf Mahmoud ‘Dj Yusuf, akifuatiwa na msanii wa bongo fleva nchini, Ali Kiba (kulia).

DSC_0409 (1)

Msanii wa Bongo fleva nchini, Ali Kiba akiimba akapela moja ya nyimbo zake wakati wa mkutano huo na wandishi wa habari (Hawapo pichani), katika mkutano huo juu ya ushiriki wake kwenye tamasha hilo linalotarajia kufanyika Februari 12 hadi 15, Ngome Kongwe, Zanzibar. kushoto kwake, ni

Mkurugenzi wa tamasha hilo, Yusuf Mahmoud ‘Dj Yusuf, akifuatiwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Busara Promotions, Simai Mohammed.

??????????

Simai, Dj Yusuf na Kiba wakiwa wameunganisha mikono kwa kusalimiana ikiwa ni ishara ya Umoja na Amani, kama Kauli mbiu ya mwaka huu ya tamasha hilo inavyohimiza amani.

??????????

Ali Kiba katika ‘Selfie’ na Mwenyekiti wa Bodi ya Busara Promotions, Simai Mohammed, muda mfupi baada ya utambulisho wa msanii huyo juu ya kupiga shoo kwenye tamasha la 12 la Sauti za Busara, litakalofanyika Februari 12 hadi 15, Zanzibar.

Na Andrew Chale

Mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ali Kiba ametamba kukonga nyoyo watu mbalimbali watakaojitokeza kwenye tamasha la 12 la Sauti za Busara linalotarajia kufanyika, Februari 12 hadi 15, Ngome Kongwe, Zanzubar.

Ali Kiba alieleza hayo leo Alhamisi, Januari 29. wakati wa mkutano wa ulioandaliwa na Busara Promotions, wandaaji wa tamasha hilo kubwa la Kimataifa linalofanya muziki wa ‘Live’,  ambapo kwa mwaka huu zaidi ya wanamuziki na vikundi 37, watatoa burudani kwenye tamasha hilo kwenye viunga vya Ngome Kongwe, Unguja, Zanzibar.

Akizungumza mbele ya wandishi wa habari, Ali Kiba alisema kwa sasa amejiandaa kutoa burudani ya aina na ambayo itakonga nyoyo kwa watu wote watakaojitokeza kushuhudia tamasha hilo.

“Hii itakuwa ni zawadi kwa watanzania wote kunishuhudia nikiimba ‘live’ bila kutumia ‘cd’ kama wafanyavyo wengine. Mimi ni mwanamuziki na nimesoma muziki hivyo nitapiga muziki wa nguvu jukwaani” alisema Ali Kiba.

Na kuongeza kuwa, kwa sasa yupo kwenye mazoezi ya muda mrefu wa kujifua na bendi maalum  kwa ajili ya shoo hiyo huku akitamba kuwa, yeye ni msanii kwani muziki aliusomea na kujifunza huko nyuma alipokuwa  katika Nyumba ya kuibua vipaji THT, ambapo alijifunza vitu vingi ikiwemo kuimba muziki wa bendi na ‘live’.

Aidha, aliwaomba wapenzi na wadau wa muziki kujitokeza kwa wingi

kushuhudia tamasha hilo kwani wasanii mbalimbali wa ndani na nje watatoa burudani ya kipekee.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa bodi ya Busara Promotion, wandaaji wa tamasha hilo, Simai Mohammed, alisema tamasha limeweza kuongeza ajira na uchumi wa Zanzibar kwani pia limeongeza fursa za utalii.

Kwa upande wake, Meneja wa tamasha  hilo, Journey Ramadhani, alisema tamasha hilo limeweza kuongeza fursa kila mwaka ikiwemo kutoa ajira kwa vijana wa kitanzania kwa asilimia 90, ambapo kwa mwaka huu wanatarajia kuwa na watendaji kazi na wa kujitolewa watakolipwa katika kusaidia tamasha hilo, zaidi ya watu 150.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa tamasha hilo, Yusuf Mahmoud ‘Dj Yusuf’ alisema tamasha hilo limeweza kuibua wasanii mbalimbali ikiwemo kujitangaza kimataifa.

Aidha, Dj Yusuf alieleza kuwa, tamasha la mwaka huu litaendana na kauli mbiu ya kuimiza Amani, pia wameandaa tuzo maalum na zawadi maalum kwa wasanii wa Tanzania watakaoshinda katika kutunga nyimbo za amani.

Mbali na Ali Kiba, Wasanii wengine Isabel Novella kutoka  Msumbiji, Ihhashi Elimhlophe (Afrika Kusini),   Tcheka (Cape Verde),   Diabel Cissokho (Senegal),  Culture Musical Club (Zanzibar),  Msafiri Zawose (Tanzania),   Aline Frazão (Angola),   Tsiliva (Madagascar),   Leo Mkanyia and the Swahili Blues Band (Tanzania),   Mohamed Ilyas & Nyota Zameremeta (Zanzibar),   Thaïs Diarra (Senegal / Mali / Uswisi),   Liza Kamikazi and band (Rwanda),   Erik Aliana (Cameroon),  Mpamanga (Madagascar),   Mgodro Group (Zanzibar),   Rico Single & Swahili Vibes (Zanzibar),   Zee Town Sojaz (Zanzibar),   Ifa Band (Tanzania) na wengine wengi. Maelezo zaidi yanapatikana katika www.busaramusic.org

MADEE (@Madeeseneda) aleta GUMZO kwenye Social Network, angalia kionjo cha video yake mpya “VUVULA”

Msanii Madee kutoka kundi la TIP TOP Connection anatarajia kuzinduz video yake mpya tarehe 7 mwezi wa 2 mwaka huu pale Mikocheni kwenye ukumbi wa ESCAPE 1. Kabla Madee hajazindua video hii jana meneja wake Babu Tale alishare na wadau kipande cha video hii kwenye Instagram na kuleta comments nyingi za watu wakilalamika kuwa video hii kuna kipande cha mwanadada anayecheza jikoni kwamba ataifanya video hii isichezwe hapa BONGO.

Haya mdau nimeona na mimi niwawekee hapa ili kionjo hiki kisiwapite na nyie


NEW VIDEO: Malfred – PIGANA (Official Music Video)


Shot in Uganda Directed by SPK filmz NextEdition

Jos Mtambo Feat. Nako 2 Nako – SIJAWAHI KUFEKI[NEW AUDIO]

Greetingz Everybody,Hope Y’all doin’ Great…We(Tongwe)are all doin’ Great,Fresh,Safe N Sound..

Thanx n Praises to The Almighty Creator…We got some New Releases  from our Untouchable Studioz,

Startin’ wit’ “JOS MTAMBO”.. He is Premierin’ his New Single tittled “SIJAWAI KUFEKI  FT NAKO 2 NAKO ”

At Tongwe studios,Oysterbay Dar-es-Salaam,from his Album named “WAKIGAMBO”…

tracks are from our Undisputable Studios,Tongwe Record…

We are Kindly asking for Your Support in Promotin these Projects,Hopin U’ll Enjoy & get

Satisfaction from ‘em..

Sincerely yours

Tongwe Recoords.


Rhymes B - Mkufu[NEW AUDIO]

Sikiliza na Download hapa Ngoma mpya kutoka Rhymes B - Mkufu


https://mkito.com/song/mkufu/12692

Nay Wa Mitego - Only One[NEW AUDIO]@paulmkale

Ninafasi yako mpenzi na shabiki wa Nay Wa Mitego Kusikiliza Ngoma Nyingine"ONLY ONE"Bofya hapo kudownload

Picha,Yemi Alade akishoot video ya ngoma yake mpya‘Taking Over Me’

Ukiangalia video yake ya ‘Johnny’ na ‘Tangarine’, au namna alivyofanya vizuri kwenye video ya ‘Baby Hello’ ya staa mwenzake wa Nigeria, Wande Coal; unaona ni jinsi gani staa huyu wa muziki Yemi Alade yuko vizuri kwenye kuifanya video kupendeza.

Ana nyimbo kali kibao, collabo pia ambazo zimefanya Afrika tumtambue staa huyu kutoka Nigeria, mpya kutoka kwake ni kwamba ametupa ishara tukae tayari kuiona video yake mpya muda wowote kuanzia sasa.

Kashea na sisi picha za Behind the Scenes, wimbo ulifanywa na Producer GospelonDeBeatz, wimbo unaitwa ‘Taking Over Me’ humo ndani kapewa collabo staa mwingine kutoa Naija, rapper Phyno.

Kingine ni kwamba video hii inafanywa Nigeria na South Africa, nimeshea na wewe hizi za Behing the Scenes.

Cannibal & Rapdamu – Friday Fever[NEW AUDIO]

Baada ya Kimya kingi kichwa cha 254 “Cannibal” charudi tena, round hii akidondosha heavy hiphop joint akiwa na Rapdamu,ngoma inaitwa “Friday Fever” ambayo iko powered na Grandmaster Records na Fresh120Media
Sikiliza na download friday fever hapa: https://mkito.com/song/friday-fever-cannibal-rapdamu/12689

@cannibalshattah @johnbgrand

Diamond Platnumz - Perfomance At Leaders Club On Tigo Kiboko Yao(VIDEO)

Tazama hapa Platinumz alivyowamaliza kwenye show aliyoifanya  Leaders Club On Tigo Kiboko Yao ni sheedah


Mona Gangstar - Okelo wa show(Officil Music Video)

Okelo wa show ni jina jipya kwenye ramani ya muziki wa B0ng0 Fleva hii ni miongoni mwa kazi zake za mwanzo utakazozifahamu,mkono mwingine wa Mona Gangstar kutoka Classic Sound,upande wa video imeongozwa na Pablo.

Bonyeza play kutazama.


Wema Sepetu (@wema_sepetu) ”IN MY SHOES” S02EP10(VIDEO)

Mwigizaji staa wa Tanzania, Wema Sepetu hukutana na watu wake wa nguvu kila wiki kupitia show yake ya TV (Eatv) inayohusu maisha yake pamoja ishu nyingine zinazomuhusu time hii amekuletea in my shoes ya msimu wa pili iliyopo katika nafasi ya kumi.

Itazame #In my Shoes msimu wa pili episode 10 kwa ku play hapa

WATU WANNE WAFARIKI DUNIA BAADA YA KULA UGALI WENYE SUMU HUKO KIGOMA

Watoto wanne wa familia moja wakazi wa kijiji cha kibambila wilayani Kakonko mkoani Kigoma wamefariki dunia na mmoja amelazwa katika kituo cha afya Kakonko baada ya kula chakula kinachosadikiwa kuwa na sumu.


Mganga  mkuu wa wilaya ya Kakonko  Dkt. Fadhil Seleman  amewataja watoto hao waliofikishwa kituo cha  afya  Kakonko kuwa ni  Neema Joseph, Jonas Joseph, Majaliwa Joseph, Yusuph Joseph wote wakiwa na umri wa kati ya miaka 11 na 18 walifikishwa hospitalini hapo  wakiwa na hali mbaya na walipoteza maisha wakati wanaendelea kupatiwa huduma. 

 

Amesema kwamba uchunguzi wa awali umeonesha kuwa watu hao wamekula sumu katika chakula cha ugali.


Akizungumzia tukio hilo baba wa watoto hao Joseph Kajolo ambaye alinusurika katika tukio hilo amesema hajui chanzo cha tukio hilo huku baadhi ya wananchi wa Kakonko  wameeleza kusikitishwa kwao na tukio hilo na kwamba vifo vya sumu katika wilaya hiyo  vimekuwa vikijirudia mara kwa mara.


Mkuu wa wilaya ya Kakonko Peter Toyima amesema polisi inamshikilia mtu mmoja kuhusiana na tukio hilo huku akiwataka wananchi kuacha vitendo vya kuwekeana sumu

Hizi hapa info za ngoma mpya ya AY"Zigo"

Elchapo aka Ambwene Yessaya aka AY anatarajia kuachia wimbo wake mpya uitwao ‘Zigo’ February 02, 2015 uliyofanywa na mtayarishaji wa muziki Nahreel na kufanyiwa mixing na Marco Chali.

AY amesema kuwa wimbo wake mpya ‘Zigo’ sio collabo, Ana collabo nyingi tayari, hii kaamua kufanya mwenyewe.

Young 60 ft One Six - Mapenzi Basi(Official Music Video)

Video: Young 60 ft One Six - Mapenzi Basi

Audio Produced by Bello Beats and D Touchz

Video Directed by Erick Backamaza

Lights and Transport manager :Jose and Amin Athuman

Model:Alice Kim Wallece

Dressed by :DILLE CLASSIC WEAR

Sponser:Precious ENT.

Family:Rap Nation

Nikki Mbishi Ft Ciana Jordan - Sikujua[NEW AUDIO]@paulmkale

Sikiliza na Download hapa ngoma mpya kutoka kwa Nikki Mbishi"SIKIJUA"Akiwa na Ciana Jordan


Wiista - Naiye (Official Music Video)

My name is Wiista this is my first single titled NAIYE from my upcoming EP. You can also download the audio on Mkito at https://mkito.com/song/naiye/9841 . This Video was Shot by Abas Adam in Bagamoyo to capture the true essence and culture around the song itself, with the help of NGOMA Entertainment (My Management) NAIYE Music video's concept was brought to life.

Adam Mchovu - Tiririka ( Official Music Video )

Adam Mchomvu anakuletea video mpya ya ngoma yake"TIRIRIKA"Iliyoongozwa na Directed Hanscana ambaye anafanya kazi yake vizuri sasa bongo,Ninafasi yako kuitazame hapa chini


J Martin Feat. Youssou N'Dour - Time Is Now (Official Music Video)

Staa wa Nigeria, J Martin time hii amekuletea hii video yake mpya inayoitwa Time is Now amemshirikisha msanii kutokea Senegal Youssou n ‘Dour.

Nakukaribisha kuitazama hapa chini mtu wangu.


Rihanna ft Kanye West & Paul MacCartney - FourFiveseconds(Official Audio 2015)

Staa wa muziki Robyn Fenty Maarufu “Rihanna” ametoa single mpya ‘FourFiveseconds‘ akiwashirikisha mastaa wenzake Kanye West pamoja na Paul MacCartney.

Tangu atoe nyimbo yake ya Jump Rihanna sasa amerudi upya na kuahidi mashabiki wake mambo mazuri zaidi ikiwa pamoja na kutoa albamu yake mpya mwaka huu


YBM Clevor Nation - Tom Boy[NEW AUDIO]

Sikiliza Ngoma Ya Wasanii wapya ambao wameweza kufanya poa kwenye game ya muziki,Pakua hapo chini ngoma hii kali

Diamond,Linex,Mwasiti,Stamina,Roma,Mwana FA,Peter Msechu,Kala Jerimiah,Keisha,Tudd N.K - Tokomeza Zero(VIDEO)

COVER PAGE 1
Wasanii maarufu wa muziki nchini wanaoguswa na hali ya elimu nchini Tanzania wameachilia video ya kipekee ya wimbo wa Tokomeza Zero wenye lengo la kuelimisha, kuburudisha na kuitaka jamii nzima kuipa kipaumbele sekta ya elimu. Wimbo huo umeimbwa na Mwasiti, Linah, Roma, Stamina, Maunda Zorro, Peter Msechu, Mwana FA, Linex, Keisha, Diamond, Kala Jeremiah.

Kundi jipya la Wakata Mkaa na Maana Yake Iko Hapa!

Maswali yamekua mengi sana vichwani kwa watu wengi wakijiuliza kuwa hii Mkata mkaa ni kundi jipya?na kama ni kundi linaundwa na watu wangapi?na vipi kuhusu Tip Top na Tmk Wanaume Family.
Temba kutoka Tmk Wanaume family wameongea  na kutoa ufafanuzi juu ya jina hili>>’Wakata mkaa tunabaki pale pale ni watu wanaofanya kazi ngumu sasa jiulize kama Mkata Mkaa amepata pesa yake anataka kurudi zake kijijini halafu wewe unataka kumdhurumu inakuaje hapo’
‘Kwa hiyo wakata mkaa ni jina jipya tulilokuja nalo lakini ni wale wale Tmk Wanaume Family lakini tumewaongeza watu wengine ambao ni rafiki zetu kama Madee,Julio ingawa utawasikia watu wengine wakiwemo Watangazaji pia wakiwa wanawakilisha Wakata Mkaa.

Benson(@gnrbenson) –Denglisch(Official Music Video)

Tazama video mpya mpya kutoka kwa

Benson(@gnrbenson) "Denglisch"

Grindnomic

Records presents:



Artist: Benson TheAfricanBoi

Song: Denglisch

Prod.: Stiggo

Mixtape: Motivation (Coming Out Soon...)

Video: Hector Schneider & Benson


DOWNLOAD TRACK FOR FREE ( *limited* ):

https://soundcloud.com/grindnomic/den...

Iyanya ft Don Jazzy - Gift[Official Audio 2015]

Iyanya anakuletea ngoma mpya "GIFT"Aliyomshilikisha Dony Jazzy waliyoirekodi katika studio ya Mavin Records.Isikilize hapa na download

R Kelly - Happy Birthday(Official Music Video)

R Kelly anakuletea video yenye mambo mengi ya ujana. Staa huyu wa R&B anaigia kwenye chumba kilicho jaa wanawake na kutojua kitu gani kilitokea usiku uliopita, video inarudi nyuma kuanzia mwanzo wa stori, Bonyeza Play kuitazama.

Video ya Adam Mchomvu"Tiririka"Kuzinduliwa J`Pili hii

Tunakutana Club Billz Jumapili hii January 25 kumsuport mtu wetu Adam Mchomvu ambaye anazindua video yake mpya.list ya wasanii ni ndefu ambao wataperfoam kuna Fid Q,Joh Makini,Mr. Blue,Nikki wa pili,Ben Pol,Young D,Shilole,Barakah Da Prince,Jay Moe,Belle Nine na wasanii wengi wakali.

Ndoa ya Sheta Yafikisha miaka miwili sasa

Shetta na mke wake Leila wametimiza zaidi ya miaka miwili kwenye ndoa yao na rapper huyo amedai kuwa ni furaha tu ndio iliyotawala familia yake.Shetta na Leila walifunga ndoa mwaka 2012 na hadi sasa wamebarikiwa mtoto mmoja wa kike aitwaye Qayllah.

Rapper huyo amesema kuwa anamshukuru Mungu kwa kumpa nguvu huku familia yake ikiwa ni yenye upendo na amani.

“Mimi nilioa huko nyuma na matunda yake ndo haya unayaona, Qayllah. Nilioa lakini sikufanya sherehe, ilikuwa kimya kimya saa kumi na mbili baada ya watu kumaliza ile swala ya saa 11 ndo ikapita. Kwahiyo Mama Qayllah ni mke wangu wa ndoa. Sikupiga picha wala nini.


Qayllah

“Watu wengi hawakufahamu kwa sababu haikuwa na shamra shamra pia sikupenda kuweka wazi mambo yangu ya kifamilia kwa wakati huo. Lakini namshukuru Mungu mpaka sasa hivi nafurahia maisha yangu pamoja na familia yangu,” aliongeza Shetta.

Picha,Mwinyi na Lowassa katika sherehe Monduli

photo 2

Rais mstaafu wa awamu ya pili Al hadji Ali Hassan Mwinyi akizindua moja ya sanamu za kumbukukumbu ya waanzishi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Maasai ambayo imeadhimisha miaka 20 toka kuanzishwa kwake,huko Monduli Mlimani, leo jumamosi 24 January.

photo 3

Mke wa mbunge wa Monduli mama Regina Lowassa akipanda mti wa kumbukumbu ya miaka 20 tokea kuanzishwa kwa shule ya sekondari ya wasichana ya Maasai wilayani Monduli leo jumamosi January 24.Anayeshuhudia ni mumewe Mh Edward Lowassa na mbunge wa Viti maalum(ccm) mkoa wa Arusha Namelok Sokoine.

photo 4

Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa na mkewe mama Regina Lowassa katika sherehe hizo

photo 5

Rais Mstaafu wa awamu ya pili al hadji Ali Hassan Mwinyi akisamiliana an mama Regina Lowassa wakati akiwasili katika shule ya sekondari ya wasichana ya Maasai wilayani Monduli ambapo shule hiyo inaadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwake.

Mrisho Mpoto - Njoo Uchukue[NEW AUDIO]@paulmkale

Mrisho Mpoto ameachia rasmi ngoma yake mpya "NJOO UCHUKUE"Ni wakati wako sasa kuisikiliza na kudownload hapa

Yamoto Band - Nitakupwelepweta(Official Music Video)

Style ya muziki wanaoufanya imewafanya kupanda mashabiki wa umri tofauti,Ninafasi yako mpenzi na shabiki wa Mkubwa Na Wanawe kutazama video yao mpya"NITAKUPELEPWETA"Iliyoongozwa na Director Adam Juma,Itazame hapa

Tazama picha ya nyumba aliyopewa mshindi wa BBA 2014,Idris Sultan


Tanzania kupitia Idris Sultan ilibuka mshindi wa shindano la Big Brother Afrika 2014, kwenye interview nyingi alizofanyiwa Idris alisema pesa nyingi atatumia kusaidi watoto Tanzania na Africa, Info mpya ni kwamba super star huyu ametumia kiasi flani cha pesa zake kununua jumba lililopo Dar es salaam maeneo ya mbezi Beach.I have seen thousands of people through my life time, got helped and expected to do alot in return, broken and crushed with no one to pick me up. I have struggled from ground level with all sorts of sayings like “you will never make it” to where i am now. I have shaken millions of hands not knowing who has good intentions with me. The world is for everyone who has a dream and a good will to it. The world is for all who want to change lives and make people smile. The world full of good hearted people is a dream. I stand today and say “my name is Idris Sultan and am not that special, that unique, that strong than most of you. I just dared to go for what i want, put my heart to it and here i am today. This is just the beginning. You’re welcome to join.” Ghalib Said Mohammed you’re a man with a golden heart i will love to be like you in a blink of an eye. Thank you for my new house. #Godbless #Alhamdulillah #GSM #dream #achieve #dare #youCan #success

Ali kiba - Mwana (Official Lyric Video)

“Mwana” is Alikiba’s most anticipated music video to date. ‘Mwana’ is Alikiba's 1st official release through his worldwide partnership with his record label and management company ROCKSTAR4000 and Rockstar Publishing. The Music Video ‘Mwana’ is the first single from Alikiba’s 3rd Album, released after a 3-year hiatus from the music scene. Alikiba describes this album as his “most personal and mature project that pushed his versatile talentand creativity to inner depths.”


Fans can also follow Alikiba on any of his social media and official digital networks:


FOLLOW ALIKIBA:


Bookings: alikiba@rockstar4000.com

Official Website: www.IamAlikiba.com

Facebook: www.facebook.com/rockstar.alikiba

Twitter: @OfficialAlikiba ortwitter.com/officialalikiba

Instagram: @OfficialAlikiba orinstagram.com/officialalikiba