Picha: Director Hascana amepost picha akiwa ametandaza mamilioni ya pesa,hii ni kutokana na ubora wa kazi yake

DIRECTOR HASCANA KULIA

Baada ya kufanya vizuri kwenye video mpya ya Vanessa Mdee & Barnaba- Siri,Director Hascana ameanza kuonyesha cheche zinazoashiria kuwa kukaa kwake nyuma ya camera kumeanza kuleta matunda.




Pia wiki hii Director Hascana amefanya kazi ya kushoot video mpya ya star wa muziki tz Diamond Platinumz ambayo wapo na Khadija Kopa ambayo inatarajia kutoka hivi karibuni.Hizi ni picha za vibunda ambavyo anamiliki Hascana kwa sasa

Soma hapa kupata taarifa zaidi kuhusiana na kifo cha Mbunge wa Mbinga KAPTENI JOHN KOMBA

Mbunge wa Mbinga Mh. Kapten John Komba amefariki dunia leo saa kumi jioni katika hospitali ya TMJ Mikocheni jijini Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa mtoto wa marehem Jerry Komba,amesema kifo cha marehemu baba yake kimetokana na ugonjwa wa kisukari ambapo amedai kuwa sukari ilishuka ghafla akiwa nyumbani kwake Mbezi Beach.

Miaka mitatu iliyopita, Komba alipelekwa nchini India alikokwenda kufanyiwa upasuaji kwenye nyonga, tatizo lililomsumbua kwa muda mrefu likichagizwa na ule unene aliokuwa nao.




Katibu wa mbunge Gasper Tumaini alisema kuwa mbunge huyo alikimbizwa katika hospitali ya TMJ na ndipo mauti yalipomkuta.


Katibu huyo alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hosp ya Lugalo jijini Dar Es salaam ambapo ratiba ya maziko bado haijafahamika.

New Music : Yuzzo - MC/Download

Hii ni release ya kwanza kubwa kutoka kwa Yuzzo kutoka kundi la Wantengwa tangia ahamie nchini Norway kuendeleza muziki wake. Pamoja na kuwa sasa anafanya muziki wa Live kwa kiasi kikubwa bado hajasahau alikotoka na hapa anakuletea wimbo wake MC (Emcee) huku akikumbushia alikotoka kwenye roots zake za Hip Hop.Download hapa pamoja na lyrics https://mkito.com/song/mc-emcee/13279

Kauli Ya Young Dee Yakera Bloggers Na Mkito Iongeze Malipo yake Kwa Bloggers wote Kama Mdau Wa Muziki Hii Inakuhusu

Ifike kipindi Wasanii wa Muziki wasijisaulishe bali wakumbuke wapi walianzia na mpaka kufika leo ni support gani wamepewa na Blogs mpaka kufika hapa.
Leo nimesoma habari kutoka Bongo5 yenye kichwa cha habari hiki "Exclusive: Young Deeatoa ujumbe muhimu kwa blogs za burudani Tanzania" Huu ni mtazamo wake kwenye kazi yake lakini ni vema angefikiri kwanza kabla ya kuwa mbinafsi.

Sipingi swala la Msanii kuuza nyimbo zake MKITO hapana cos hiyo ni haki yake, lakini kabla msanii hajaanza kuangusha lawana kwanza angejiuliza tatizo lipo wapi? naamini wao ndio wangekuwa watu wa kwanza kuwatetea Bloggers ili nao waboreshewe malipo yao kama vile ambavyo wao wanapokea hizo Millioni zao. Badala yake unakuta Msanii anajitoa fahamu na kuanza kuongea kwamba hataki nyimbo zake ziwekwe sehemu nyengine zaidi ya MKITO sasa mbona wakati tunasambaza na kuwekeza nguvu kwenye promo ya nyimbo zenu bila hata kutoa Senti 5 hamkuwa na kauli mbovu hivi?!
Naheshimu sana kazi ya Msanii maana ndio kitu kinachompa kula, lakini ifike wakati Wasanii nao waheshimu Blog na mitandao mingine yote ambayo ina support kazi zao kwa namna moja ama nyengine.

Wiki chache zilizopita aliyekuwa Editor wa Blog hii alitumiwa wimbo wa Gosby - Noma ili kupandishwa kwenye Blog naye alichukua wimbo huo na kuupandisha lakini hakutumi link ya Mkito, baada ya masaa kadhaa nikapokea simu kwa mtu ambae ana uhusiano na Gosby na kuhoji kwanini haijatumika link ya Mkito? Nilijaribu kumuelewesha kwanza Editor hakuwa anaelewa chochote kuhusu Mkito pili Nilijaribu kumuelewesha kuhusu mfumo mzima wa malipo na yeye akanijibu hakujua hilo nikamwambia ni vema wasanii nao waangalie upande wa Blogs ambazo ndio source kubwa ya kuingiza hizo pesa nao at least walipwe vizuri lakini hiyo story iliishia hapo na sijui kama aliwekea maanani jambo hilo.

Pia Mkito nao wabadili mfumo wao maana sidhani kama unamfaidisha Msambazaji (Blog) bali unazidi kumuumiza, unakuta malipo yanayoenda kwa Blog inayopost wimbo ni Tshs. 3 tu kwa download moja sasa kwa hesabu ya haraka haraka tu zidisha hiyo Tshs 3 kwa Download 1,000 unapata 3,000 ambazo kwa Mkito kuzipata ni ngumu sana kutokana na mfumo wao wa ku download wimbo. Tunaambiwa kwamba tunalipwa kwa asilimia bila kuoneshwa mkataba wa malipo ambayo kampuni inayotangaza imelipa kiasi kadhaa hivyo kutokana na mgawanyo wa kiasi hicho blog itapata hiki, Msanii hiki na wao wenyewe watabaki na asilimia zao, lakini tunalazimishwa kuamini hata kama sio kweli.

Ifike muda Bloggers tuthaminiwe kwa kile ambacho tunafanya, na vitu kama hivi ndio vinasababisha ugumu kwa wasanii chipukizi kutoka au ngoma zao kufika sehemu nzuri, kama kungekuwa na mfumo ambao unafaidisha pande zote naamini wasanii chipukizi wengi wangefurahi maana wangesikika kirahisi bila changamoto yoyote ile.

Najua wengi wanatamani kuongea mengi kuhusu hii issue na kutoa madukuduku yao bali nidhamu ya woga inachangia, Najua baada ya post hii wapo ambao watachukia na kuchukua maamuzi wanayoyajua wao pia wapo ambao watanielewa na kujua tatizo lipo wapi.
Asante.

New Video: Chidinma – Kite(Official Music Video)

Tazama hapa video mpya ya mwanadada Chidinma kutoka Nigeria,Ngoma iitwayo"KITE"Shot in Cape Town South Africa, Directed by award winning cinematographer Clarence Peters. (TheGoretti Company & CAPital Hill Music)

New Video: Hemed PHD – Far Away(Official Music Video)

Tazama hapa Official Video ya msanii HEMED PHD. Nyimbo inaitwa FAR AWAY na audio imetengenezwa na SEI wa SEI RECORDS. Video imefanywa na KWETU STUDIOS, Directed by Msafiri Shabani.

New Music: Ali Kiba - Chekecha Cheketua/Download

Mkali wa Bongo flava Ali Kiba Anakuletea rasmi time hii ngoma yake mpya"CHEKECHA CHEKETUA"Ninafasi yako sasa shabiki na mpezi wa muziki Kusikiliza na kudownload hapa kichupa hiki kikali ile mbaya.Ngoma imetayarishwa na Studio Cheidaz Record@paulmkale

New Video: Jambo Squad - Shigidi(Official Music Video)

Hii ni video mpya kutoka kwa Jambo Squad iitwayo"SHIGIDI"Ikiwa ni Remix ya Shekin,Itazama hapa

New Music: Jambo Squad - Shigidi/Download

Sikiliza na download hapa ngoma mpya ya Jambo Squad"SHIGIDI"

Collabo nyingine aliyoshirikishwa Ali Kiba na msanii wa bongo fleva.

Msanii Tunda Man amethibitisha kuwa amefanya wimbo wa Ali Kiba na ndio unaofata baada ya video ya Achana na mimi. Tunda Man amesema wimbo aliofanya na Ali Kiba utaitwa ‘Baby‘. Hii itakuwa mara ya pili Tunda Man anafanya kazi na Ali Kiba baada ya ‘Msambinungwa‘.

New Music: Chriss Wamarya – Nazisaka/DowNload

Sikiliza hapa na Download wimbo mpya wa Chriss wa Marya"NAZISAKA"

New Videi: Jua Cali - Karibu Nairobi(Official Video)

Jua Cali anakuletea video ya ngoma yake mpya "KARIBU NAIROBI"Ninafasi yako kuitazama hapa video hii iliyoongozwa na Dir-Director: @vjone,Producer: Beat Ya Keggah

New Video: Tanchy – Mabawa (Official Music Video)

Tazama hapa video mpya kutoka kwa  Tanchy anakwambia"MABAWA"


Kaa Tayari;Ali kiba kuachia ngoma mpya"CHEKECHA"Hapo kesho


Baada ya mwaka jana 2014 kuuvunja ukimya uliotawala kwa miaka mingi kwa kuachia single ya ‘Mwana’, Alikiba anategemea kutoa wimbo wake mpya wa 2015. Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii Alikiba ameshare cover za wimbo mpya uitwao ‘Chekecha’ unaotarajiwa kutoka Ijumaa Feb 27. Wimbo huo umefanyika kwenye studio ya Combinenga chini ya producer Man Walter,Ungana nami hapa kupata ngoma mpya ya Alikiba hapo kesho@paulmkaleLeo Feb 25 kupitia instagram  ame teaser kava mbili ambazo zikidhihirisha ujio wa single mpya, kava moja ilikuwa imeandikwa Cheketua na la pili imeandikwa Chekecha.

New Video : Future Jnl - Without You (Official Music Video)

Mkali wa miondoko ya RnB kutoka Rock City,Mwanza '*Future Jnl' *ameachia rasmi video ya wimbo wake mpya *" Without You"* Muongozaji wa Video ni Msafiri Shabani kutoka Kwetu Studios. Ninafasi yako sasa kuitazame hapa

Picha: Alikiba akishoot video katika mbuga za wanyama Tarangire


Muimbaji wa "Mwana" Ali Kiba aliyekua miongoni mwa wasani waliotumbuiza kwenye tamasha la sauti za busara mwaka huu,Leo akiwa na timu yake ya Rockstar4000 wametia timu katika mbuga za wanyama ya Tarangire iliyopo mkoani Manyara.Na amepost baadhi ya picha akiwa katika viota vilivyomo kwenye Mbuga hiyo,Hatujajua nini anafanya ila tuendelee kusubili@paulmkale

Alikiba akichukua baadhi ya picha kwenye mbuga hiyo

Yusup Mlela na Esha Buheti kutia timu Marekani kwa ajili ya Kufanya Filamu

Esha Buheti  amesema kuwa yeye na Yusuf mlela wamepata nafasi ya kwenda Marekani kufanya filamu. Steve Nyerere aliandika Instagram Nawatakia safari njema ndugu zangu mungu awatangulie kwa kila jambo najua mungu ndio anayepanga kuna mengi ila hili limeanza kwenu na milango mnaifungua wazi msiwe kama wangine wenye kucheka machoni uku moyo umekunjama. Hahahahaha.alianza wastara . Mona . Sasa zamu yenu mlela na Esha mkatuwakilishe vyema . USA .

New Video: Future - Codeine Crazy (Official Music Video)


Wewe ni shabiki wa rapper Future? time hii amekuletea hii video mpya ya single yake ‘Codeine Crazy’ ambao unapatikana kwenye mixtape yake inayofahamika kwa jina la Monster.

New Music: Tanzania Female Artist - Simama Nami/Download

Huu ni wimbo maalumu ulioimbwa na wasanii wa kike kutoka TANZANIA, wimbo huu unahusu janga la mauaji la ALBINO nchini Tanzania na duniani kote. Wimbo umeimbwa na wasanii hawa 1. Kajala (Bongo Movie), 2.Shamsa Ford (Bongo Movie), 3. Keisher (Bongo Flava Artist) 4. Mwasiti (Bongo Flava), 5. Linah (Bongo Flava), 6. Grace Matata (Bongo Flava), 7. Jack Wolper (Bongo Movie), 8. Irene Uwoya (Bongo Movie) 9. Shilole (Bongo Flava/Bongo Movie) 10. Khadijanito (Bongo Flava) 11. Zamaradi (Mtangazaji wa Radio) Powered by paulmkale.blog.com@paulmkale

New Video: Makomando - Sherie Koko(Official Music Video)

Tazama hapa video mpya ya Makomando "SHERIE KOKO"


Collabo kati ya Sheta na msanii Wa Nigeria Kcee inanukia soma hapo

Ukizungumzia miongoni mwa wasanii wa Tanzania ambao nyimbo zao huchezwa hadi kuingia kwenye Top 10 za radio Nigeria basi Mkali wa hit single ya Kerewe, Sheta lazima awepo kwenye list yako.

Shetta ambaye kwasasa yupo Afrika Kusini ameonekana akiwa na mkali wa hit single ya Limpopo, Kcee kwenye maandalizi ya video mpya lakini bado haijajulikana  video hiyo inayotengenezwa ni ya nani.

Siku chache zilizopita kupitia instagram, Kcee alipost picha akiwa na Shetta na kuandika;…“Work mode: on set with my bro @Shettatz no time…”—- @


New Music: Suma Mnazareti - Kimeo/Download

Suma Mnazareti ankuletea ngoma yake mpya"KIMEO"Iliyotayarishwa na Prod-Zest,ninafasi yako kubofya hapa kusikiliza na kudownload ngoma hii

New Video: French Montana ft. Jeremih - Bad B*tch(Official Music Video)

French Montana na msanii wa rnb Jeremih wametoa saluti kwa wanawake wote wazuri kupitia wimbo wao wa “Bad B***h” video ambayo imebarikiwa na sra za mastaa Travis $cott na Lil Durk.

Wimbo upo kwenye cd ya French inayotarajiwa kutoka  Mac & Cheese. Kwenye album atasikika Kanye West,Gucci Mane, Lil Wayne na Rick Ross.

New Video: Wiz Khalifa feat. Ty Dolla $ign & Chevy Woods - Still Down(Official Video)

Rapa Wiz Khalifa amewakilisha watu wake kwenye video mpya ya “Still Down,” single kutoka kwenye album ya Blacc Hollywood. Video yenye dakika sita inaonyesha ushuhuda kutoka kwa watu wake wa karibu kama Taylor Chevy Woods na Ty Dolla $ign, wakizungumza kuhusu maisha yai na Wiz Khalifa.

New Video : Belle 9 Feat Joh Makini - Vitamin Music(Official Music Video)

Bell 9 anatuletea video yake mpya ya wimbo ule"VITAMIN MUSIC"Ambayo amemshilikisha Rapper Joh Makini,Produced by Mona Gangstar - Classic Sound,Directed by Khalfan Bamushka.Ninafasi yako sasa kuitazama hapa

New Video: PSquare ft. Don Jazzy – Collabo(Official Music Video)

Tazama hapa video ya wimbo wa kwanza wa P Square na boss wa Mavins Records ‘Don Jazzy’ uliopewa jina ‘Collabo’, Video imetayarishwa na   Jude Okoye pamoja na Clarence Peters,  Video imefanyika Afrika Kusini.Itazame hapa

P-Square finally release the long awaited video to arguably the biggest song off their recent album, "Collabo". Nothing short of an archetypical P-Square video, the flick which also features Don Jazzy, is a classy pictorial with a brief comic storyline about it. Shot in SA on different beautiful and crisp scenes, the Clarence Peters / Jude Okoye directed video is nothing but top notch. Buy "Collabo" on iTunes:- https://itunes.apple.com/us/album/col... Curated by http://www.freemedigital.com

Tazama Picha: Sheta,Kcee, Nahreel, Joh Makini wapo Afrika Kusini


Wasanii Joh Makini, G Nako, Jux, V Money, Sheta na Nahreel wako nchini Afrika Kusini wakufanya shughuli tofauti za muziki wao. Joh Makini alionekana Studio na Rapa KO na kunauwezekano wa collabo kufanyika ingawa alisema ni mapema sana kuongelea.







New Music: J Deal Music - Na Mimi Nimo/Download

Sikiliza na download hapa kichupa kipya kutoka kwa J DEAL MUSIC

nyimbo iitwayo"NA MIMI NIMO"

New Music: P-Unit ft Yemi Alade - Different/Download

P Unit

(@PUNIT_KENYA)

wakuletea ngoma yao mpya"DIFFERENT"Wakiwa na mwanadada kutoka Nigeria Yemi Alade

(@yemialadee)

,Isikilize hapa na Download@paulmkale

New Video: Alicios Theluji - Loved By You (Official Video)

Moja ya hits zilizowahi kufanya vizuri East Africa ni hii collabo ya ALICIOS feat. JULIANA KANYOMOZI‘Mpita Njia’.

Alicios ni raia wa Congo ambaye anaishi Kenya, moja ya sifa kubwa na za kipekee alizonazo ni uwezo wake kuimba kwa lugha nne tofauti, kiingereza, kiswahili, kilingala na kifaransa.

Hapa nakusogezea video ya wimbo wake mpya, ‘Loved By You’ uliofanya na director Johan Lundstane.Itazame hapa

New Music: Izzo B feat Shaa - Kidawa/Download

Sikiliza hapa na Download audio ya ngoma mpya ya Izzo B"KIDAWA"Akiwa na mwanadada Shaa

New Video: Izzo Bizness feat Shaa - Kidawa (Official Music Video)

Izzo Bizness(@izzo_bizness) Rapper kutoka Green City Mbeya, anakuletea video ya wimbo wake mpya ‘Kidawa’ ambao kamshirikisha Shaa. Wimbo umetayarishwa na producer Dupy wa Uprise Music na mastering imefanywa na Master J wa MJ recordsin Dar es Salaam, Tanzania. Video imeongozwa na director aliyefanya video nyingi za Izzo, Nick Dizzo.Itazame hapa sasa.

New Video : Madee ft Raymond - Paulina (Official Music Video)

Watch brand new music video "Paulina" by Tanzanian artist Madee featuring Raymond. SUBSCRIBE Mziiki For Best African Music | http://bit.ly/MziikiTube
Like us on Facebook: https://www.facebook.com/mziiki
Follow us on Twitter: https://twitter.com/Mziiki
Circle us on G+: https://plus.google.com/+Mziikiapp
Stream music free at our official Website: http://www.mziiki.com
Visit MziikiTube channel for unlimited entertainment: http://www.youtube.com/MziikiTube

New Music: Mike Tee Ft. Rossie M - Ningejua Mapema | Download

Sikiliza hapa na download wimbo mpya wa Mike Tee FEAt. Rossie M"NINGEJUA MAPEMA"

Video :Yamoto Band wakizungumza na Charles Hilary katika BBC Dira ya Dunia


Tazama hapa Yamoto Band walipokua wakizungumza na  Charles Hilary katika BBC Dira ya Dunia Nchini Londan