Cooming Soon New Song: Diamond Platinumz - #Simba

diamond afrimaDiamond kuachia wimbo wa kurap uitwao ‘Simba’Staa wa muziki Diamond Platnumz amejipanga kuachia wimbo mpya wa kurap uitwao Simba. Akizungumza katika kipindi cha XXL cha Clouds FM Ijumaa hii, Meneja wa msanii huyo, Babu Tale alisema wimbo huo utakuwa sio wa biashara bali ni zawadi kwa mashabiki. “Kama Hip Hop ni biashara Diamond amefanya wimbo wa kurap lakini hatujauchulia kama ile biashara.Wimbo umeshaisha bado tu kuuachia,kwa hiyo mashabiki wangu wakae mkao wa kula.

Yanga yasonga mbele klabu bingwa Afrika

????????????????????????????????????
Mabingwa wa soka Tanzania Bara na wawakilishi katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga SC leo imefanikiwa kuitoa Cercle de Joachim ya Mauritius kwa jumla ya mabao 3-0, kufuatia ushindi wa 2-0 jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mchezo wa kwanza ilishinda bao 1-0.
Alikuwa ni Amissi Joselyn Tambwe, mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi ambaye aliifungia Yanga bao la kwanza katika dakika ya tatu ya mchezo kwa kichwa akimalizia kwa uzuri krosi ya winga Simon Msuva.
Yanga waliendelea kulishambuliwa lango la wapinzani wao lakini kukosekana kwa umakini wa washambuliji wao kuliwanyima magoli mengi zaidi.
Mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika Yanga walikuwa na akiba ya bao 1-0.
Kipindi cha pili Yanga waliingia na nguvu mpya na kufanikiwa kuongeza bao la pili lililofunga na Thaban Scara Kamusoko mnamo dakika ya 56 kwa shuti kali akiwa nje ya boksi, baada ya kuanzishiwa mpira wa adhabu na beki Mwinyi Hajji Mngwali.
Kwa matokeo haya Yanga sasa itakutana na APR kutoka nchini Rwanda baada ya kuwatoa Mbabane Swallows ya Swaziland kwa jumla ya mabao 4-2 katika Raundi ya Pili.
Yanga: Ally Mustafa ‘Barthez’, Juma Abdul, Mwinyi Hajji, Kevin Yondani, Vincent Bossou, Mbuyu Twite/Pato Ngonyani dk46, Simon Msuva, Thabani Kamusoko, Amissi Tambwe, Malimi Busungu/Paul Nonga dk46 na Deus Kaseke/Godfrey Mwashiuya dk76.
Cercle de Joachim: Abrefa Godfrey Yaw, Buckland Jimmy Hendrick/ Laretif Stan dk83, Balisson Paschal Damien, Natrey Isaac, Bazerque Desire, Permal Cedric, Langue Jean Anderson, Rasdarising Bhavish/Maguy Jacque Daniel dk78, Pithiaj Louis Fabien, Odame Abraham na Chiffone Louis Guiyano

Baada ya Rich Mavoko Kukana Kutoka Kimapenzi na Gigy Money, Gigy Aanika Chat zao

Baada ya video queen Gigy Money kudai kuwa aliwahi kutoka kimapenzi na Rich Mavoko na baadae staa huyo wa wimbo ‘Pacha Wangu’ kukanusha, Gigy Money aweka wazi chati zao za WhatsApp.

Gigy Money, alipost instagram chat hizo na kila moja kuiandika ujumbe wake. Hata hivyo baade alizifuta post hizo.


“Mimi mwenyewe sikujui vilevile” aliandika Gigy.


“Ahahhahaha unajua mavoko ntakudhalilishaaa ….mm ni mkimyaaa tu sio Mpole ata kidogo …unajikuta umenisahau bwege ww” aliandika Gigy.


“Banduguuuuuu kujichubua kwako ndio nkuogope weeee Richard wewe umeombaaa watu wanipigie nisikutie aibu sasa unaletaaa utoto sina nachokipoteza kumbukaaa I don’t care��������” aliandika Gigy