RAIS wa Akudo Impact, Tarsis Masela
anaendelea kuachia vitu vipya nje ya bendi yake, kama sehemu ya
maandalizi ya kukamilisha albam yake binafsi
.Baada ya kuachia audio na video ya wimbo wake mkali “Tabia Mbaya” alomshirikisha Mzee Yussuf, Tarsis Masela sasa amekuja na kitu kipya kinachokwenda kwa jina la “Chaguo Langu“. Katika kuonyesha kuwa amepania kushuka na vitu vilivyojaa viwango, Tarsis Masela hivi karibuni alikwenda jijini Nairobi nchini Kenya kuandaa video ya wimbo huo kupitia kampuni ya E-World Productions Films chini ya mtayarishaji wake Papa Vir ambaye pia ni mtangazaji.
Tarsis ameiambia DJChokaMusic kuwa
amekwenda Kenya kufuata viwango na kuleta utofauti. “Papa Vir ni
mtayarishaji wa kimataifa, nina imani video hii italeta mapinduzi kwenye
muziki wa dansi,” alisema Tarsis Masela.
No comments:
Post a Comment
paulmkale