Wimbo wa Bracket ‘Alive’ ft. Diamond ni wa shukrani baada ya memba wake kupona Kansa, Vast aelezea jinsi alivyougua hadi kupona
Alive -“Hii ni hadithi ya kweli ya Vast Bracket, safari yake hadi
alivyopona kansa mwaka 2013. Huu ni wimbo wa shukrani kwa kumfanya
mshindi aliyeishinda kansa.”
Hayo ni maneno yanayoonekana mwanzoni mwa video ya wimbo mpya ya
kundi la Bracket kutoka Nigeria iliyotoka wiki hii, ambao
wamemshirikisha Diamond Platnumz na Tiwa Savage.
Kipindi Vast anaumwa kansa
Memba wa kundi hilo aitwaye Vast, mwaka 2013 alikuwa akipigania uhai
wake baada ya kuugua kansa ya damu ambayo baadae alifanikiwa kupona,
ndio sababu ya kundi hilo kuamua kurekodi wimbo huu ‘Alive’ kwaajili ya
kumshukuru Mungu kutokana na kumuwezesha msanii huyo kupona.
“There was a time that I felt I would die. My only fear was that I was
not close to God. I was afraid that if I died, I would not make it to
heaven. We musicians have a particular lifestyle. You may plan to be
upright, but when you go into entertainment business, it would change
you.
No comments:
Post a Comment
paulmkale