Kaa Tayari;Mrisho Mpoto kuachia wimbo mpya ‘Njoo Uichukue’
Msanii wa muziki wa asili, Mrisho Mpoto anatarajia kuachia wimbo mpya uitwao ‘Njoo Uichukue’Mpoto, amesema wimbo huo utawafungua watu
macho na kuwapa mwanga kuvifuata vitu vizuri wanavyovihitaji.
“Mpaka sasa naendelea kuwepo kwenye muziki ni kwa sababu ya mashabiki
wangu. Wasikilizaji wangu au mashabiki wangu wana uwezo mkubwa wa
kutafakari nyimbo zangu mpaka wakati mwingine wananishinda mimi
mwenyewe, ndio maana wakati mwingine wananipa kazi ya kukaa mwaka mzima
kuwafikiria nitawapa kitu gani,” amesema Mpoto.
“Kwahiyo mimi naamini huu wimbo utawafungua watu na kuwapeleka kwenye
vitu wanavyovihitaji. Wimbo utatoka Jumatatu ijayo na umetengenezwa
ndani ya studio yangu.”
No comments:
Post a Comment
paulmkale