Hizi ndizo picha za utengenezaji wa video mpya ya kupinga mauaji ya albino , iitwayo #SimamaNami

Madam Ritha, Kajala, Mtangazaji Dida,Shadee,Sauda Mwilima,Zamaradi,Shilole,Mwasiti na mimi mwenyewe ni baadhi ya watu maarufu wa kike kutoka sekta mbalimbali waliojitokeza kumuunga mkono msanii Keisha katika utengenezaji wa video ya wimbo wa 'Simama Nami'.Wimbo huo unabeba jina la Kampeni yake ambayo inahamasisha jamii kuacha mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Msanii Keisha 

Shughuli ilianza kea make up kwa wasanii hao ambapo Diana wa American Nails ndo alikuwa anasimamia mpango huo kuhakikisha kila mtu atakayeonekana anapendeza.

Mimi,Grace Matata na Princess

Princess na Queen Darleen

Mwasiti na Princess

Keisha alisema Wimbo wa 'Simama Nami' ni awamu ya kwanza ya kampeni hiyo.Kwani amesema anaona kama Serikali haiko seriuz na swala la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi hivyo ameamua kujitoa ili kuwatetea wenzake

No comments:

Post a Comment

paulmkale