Staa wa Bongo Fleva,Ali Kiba amefunguka kuwa hafurahishwi na timu za mashabiki zinazojiita ‘TeamDiamond na TeamKiba’ambazo zipo kwenye mitandao ya kijamii hasa Instagram na Facebook. kwasababu Team hizo ndizo zinazokuza mambo ya ugomvi mkubwa baina yake na msanii mwenzake (Diamond Platinumz) kama ambavyo mashabiki wanadhani.Lakini Ali kiba amedai hana ugomvi na msanii mwenzake .
Akizungumza na Leo Tena ya Clouds Fm,alisema kuwa
wao ni vioo vya jamii na wanapendwa na watu wengi na anapoona yanatokea
mambo hayo kwenye mitandao hiyo ya kijamii hawezi kufanya chochote na
kuwaingilia mashabiki hao.
‘’Kiukweli sifurahishwi na timu hizi na naona kinachoendelea kwenye
mitandao lakini siwezi kufanya chochote na kuwaingilia mashabiki,ila
ushauri wangu ni bora wangeacha tu,’alisema Kiba.
Endelea kungana nami kwa Stori zingine pale zinapojiri,
No comments:
Post a Comment
paulmkale