Ushauri wa Ali kiba kwa Mashabiki, kuhusu Team za Mitandaoni:

Staa wa Bongo Fleva,Ali Kiba amefunguka kuwa hafurahishwi na timu za mashabiki zinazojiita ‘TeamDiamond na TeamKiba’ambazo zipo kwenye mitandao ya kijamii hasa Instagram na Facebook. kwasababu Team hizo  ndizo zinazokuza mambo ya  ugomvi mkubwa baina yake na msanii mwenzake (Diamond Platinumz) kama ambavyo mashabiki wanadhani.Lakini Ali kiba amedai hana ugomvi na msanii mwenzake .
Akizungumza na Leo Tena ya Clouds Fm,alisema kuwa wao ni vioo vya jamii na wanapendwa na watu wengi na anapoona yanatokea mambo hayo kwenye  mitandao hiyo ya kijamii hawezi kufanya chochote na kuwaingilia mashabiki hao.
‘’Kiukweli sifurahishwi na timu hizi na naona kinachoendelea kwenye mitandao lakini siwezi kufanya chochote na kuwaingilia mashabiki,ila ushauri wangu ni bora wangeacha tu,’alisema Kiba.
Endelea kungana nami kwa Stori  zingine pale zinapojiri,

No comments:

Post a Comment

paulmkale