Wakati
Watu wakiwa na hamu ya kupata matokeo ya tuzo za MTV ambazo Diamond ni
mmoja wa washiriki katika Tuzo hizo Diamond anazidi Kupata nafasi
zaidi baada ya kutajwa katika tuzo za African Entertainment Awards za
Nchini Marekani.
Diamond
amekuwa nominated katika vipengele viwili ambavyo ni Hottest
Male(Msanii bora wa kiume) na Single Of The Year(wimbo bora wa
Mwaka-Ntampata Wapi).
Diamond
amepost katika mtandao wa Instagram akitoa shukran zake...ameandika
"Naomba niwashkuru wadau na Mashabiki zangu wote kwa support kubwa
mnayozidi kunipa... Niwashkuru wote mlokuwa Mkihamasisha na kupiga kura
katika tunzo za #Mtvmama2015 Hakika ni upendo Mkubwa..kijana wenu now
nimetua South Africa tayari kwajili ya Kujiandaa kwa show nk... ila pia
wakati nimetua nimekutana na Habari nyingine nzuri...kuwa Nimechaguliwa
kwenye Tunzo za Marekani ziitwazo @AfricanEntertainmentAwards Kama
Msanii Bora wa Kiume Africa na Nyimbo bora ya Africa #NtaMpataWapi Hii
ndio Account yao @AfricanEntertainmentAwards Ntawajuza namna ya Kupiga
kura Soon".
No comments:
Post a Comment
paulmkale