Haya ndo majibu ya Ommy Dimpoz Kuhusu picha alizopiga na Wema X wa D

Msanii wa bongo fleva, Ommy Dimpoz, amefunguka kuhusiana na picha zilizozua utata na kuzozagaa mitandao zikimuonesha akiwa kitandani na msanii wa filamu Wema sepetu.

Ommy amesema kuwa hana maelezo zaidi ya kuzungumza zaidi ya kusema kuwa hajui ni muda upi zilipigwa picha hizo.

Wiki hii picha hizo zilisambaa mitandaoni na kuzua maswali kuwa Ommy Dimpoz, ameamua kujiweka kwa Wema, baada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Diamond Platinum."Ni picha tu mimi naona kama ni picha zingine tu za kawaida, sasa nimeshindwa kuelewa kwanini labda zimetengeneza sana stori kwasababu mimi naona sio mara yangu kwanza kupiga picha na Wema hata uki google utaona tunapicha nyingi sana kwa hiyo sijaelewa kwanini zimeleta stori

May be nafikikiri zilizotengeneza stori zaidi ni hizi ambazo zinaonesha tuko chumbani kwasababu mimi nilikuwa nimelala kiukweli na tulikuwa tunakaa kwenye apartment moja nilikua nimeshtukia picha zipo kwenye mitandao unajua unavyokaa kwenye apartment kwasababu tulienda kwenye matembezi binafsi na washikaji wengine tulikua wengi wengi kidogo tulienda South Africa unajua mnavyokaa kama familia kunakuwa na mambo ya utani utani nimeshtukia tu picha zimeenea kwahiyo hata watu wakiniuliza ninawambia wamuuliza aliyepiga picha hizo," Alisema Dimpoz.

Wengi wanafahamu kuwa wewe ni mshikaji wa Diamond Platnumz imekuaje sasa hivi kuonekana kwenye picha na Ex wa Diamond Platnumz,Wema Sepetu…?”

Ommy Dimpoz ; “…Sidhani kama kuna tatizo kwasababu hawa wote ni watu wangu nimefahamia nao siku nyingi nimekuwa nao karibu katika kipindi tofauti kabla hawajakuwa kwenye uhusiano mimi tayari ni watu wangu sidhani mimi nianze kuelezea sijui ooh nilikuwa labda na Wema sehemu, Wema ni mshikaji wangu tangia siku nyingi kwa hiyo hata kama alikuwa katika uhusiano na Diamond yakatokea mahusiano yao pengine hayapo sasa hivi hayawezi kunifanya mimi kuharibu ushikaji wangu kwasababu hivyo ni vitu vyao personal…"Alisema.


No comments:

Post a Comment

paulmkale