Chege na Temba waingia studio Afrika Kusini kurekodi wimbo na Uhuru
Wasanii wa TMK, Chege na Temba wako nchini Afrika Kusini ambako
wameenda kufanya show kwenye miji ya Pretoria na Johannesburg wakiwa na
wasanii wenzao Madee pamoja na Julio.Meneja wa wasanii hao Said Fella wamethibitisha kuwa wakiwa
huko Temba na Chege wamefanikiwa kuingia studio na kurekodi ngoma na
Uhuru waliotengeneza hits nyingi ikiwemo ‘Khona’ ya Mafikizolo, pamoja
na Ole Themba ya Linah kwa hapa Bongo.
“Kikubwa ni kwamba Temba na Chege walifanya show kwanza Pretoria,
wakaja kufanya show Johannesburg baadae tukapanga mipango wafanye ngoma
na Uhuru, kwahiyo walifanya jana ila leo wanamalizia”.
Fella amesema wimbo huo hawajamshirikisha mtu yeyote, na kuhusu kufanya video huko amesema, “ndo tunafikiria kwasababu Adam yuko kule tulikuwa tunafikiria tufanye na Adam au tufanye na nani”.
No comments:
Post a Comment
paulmkale