Funga Mwaka Mkali Wa "PACHA WANGU"Rich Mavocco Kuja Na Ngoma Kali
Baada ya kuachia ‘Pacha Wangu’, Rich Mavoko amesema yupo chimbo kuandaa silaha za kufunga mwaka.
Mavoko amesema kuwa sababu inayomfanya aachie wimbo mpya ni
baada ya kuona mashabiki wa muziki wake bado wanahitaji mawe zaidi
kutoka kwake.
“Kuna kazi ipo ndani imeshafanyiwa kila kitu, manejimenti wapo kwenye
maandalizi kwaajili ya uzinduzi. Mimi nahisi inaweza ikatoka kufunga
mwaka na pia kama tukiona vipi inaweza ikatoka kufungulia mwaka.”
amesema Mavoko.
Katika hatua nyingine Mavoko amesema mwaka huu umekuwa wa neema zaidi kwake.
“Mwaka huu umekuwa vizuri sana kwenye biasahara ya muziki wangu,
kwahiyo tunajipanga na kuomba Mungu mwakani uwe mzuri zaidi. Kuna mambo
makubwa nimeyafanya mwaka huu lakini siwezi kuyaweka hadharani bado
haijaisha. Lakini mambo yako vizuri, vikiisha watu wataviona.”
No comments:
Post a Comment
paulmkale