Kaa Tayari;J`Mosi Hii Kundi La WEUSI Kuzindua Video Za 5 Mpya Pale Dar
Familia ya Weusi inaendelea kuonesha matunda ya muungano wao, wakiwa
wanaendelea na ziara ya show zao za Funga mwaka, wiki hii Weusi
wanatarajia kuzindua video zao tano kwa mpigo pale Escape One, jijini
Dar es salaam.
Msemaji wa kundi hilo Nikki Wa Pili amezitaja video watakazozindua
Jumamosi hii November 29, kuwa ni video yake ya ‘Sitaki Kazi’
iliyofanywa Arusha na director Mkenya Enos Olik. Video ya ‘I See Me’ ya
Joh Makini iliyofaywa Nairobi na Olik, Video ya ‘Mavijanaa’ ya G-Nako
iliyofanywa Arusha na Olik.
Nyingine ni video ya Joh Makini ‘XO’ iliyofanywa na Nisher , pamoja
na video nyingine ya G-Nako inaitwa ‘Morale’ imefanywa na Halfani.
“Zote tano tutazizindua Jumamosi Escape One katika Funga mwaka la
weusi jijini Dar es salaam.Sio mchezo si unajua game linabadilika
kwahiyo formula na zenyewe zinabadilika kila siku.” Nikki ameiambia 255 ya XXL ya Clouds Fm.
No comments:
Post a Comment
paulmkale