Weusi kujenga maktaba 100 ndani ya vijiji 100 kupitia kampeni ya "Mia Mia Mwanangu"

Kampuni ya Weusi yenye members 5, Joe Makini, Gnako, Nikki wa pili, Bonta na Lord Eyes, imeazimia kujenga maktaba 100 katika vijiji 100 kwa kushirikiana na watanzania wengine.Kampeni itakayofanikisha kujengwa kwa makataba hizo 100 katika vijiji 100 ambazo zitakuwa na vitabu 100 itakuwa inaitwa "MIA Mia Mwanangu" kampeni ambayo itamuhamasisha mwananchi wa kawaida mwenye kipato cha chini kushiriki katika kuleta mabadiliko kwa yeye pia kuchangia shilingi 100, kwahiyo ni kampeni ambayo itachangisha shilingi 100 tu kutoka kwa mtanzania kwa ajili ya kufikia azimio hilo

unajua kwasababu sisi tunafunga mwaka na tunakutana na mafans wetu wote wanaotuunga mkono sehem zote, kwahiyo na sisi tumekaa tukafikiria tufanye kwaajili ya ku-give back to the community. Toka zamani mi nilisemaga mi nna idea yangu ya kijiji cha taaluma, ambacho nilisema ni kutambua machimbo ambayo yapo uswahilini ambayo wanafunzi wanasoma na kuya-facilitate, lakini sasahivi nikaona hii idea nii-extend nikatafuta msemo ambao uko uswahilini wa vijana wa kawaida wa watu wa chini kabisa......." amesema Nikki wa pili


"Nimebuni hiyo kampeni inayoitwa MIA MIA MWANANGU, ni kampeni rahisi sana tutajaribu kuhamasisha kila mtu mwenye uwezo wa kuchangia shilingi 100 ambayo nafikiri ni hela ndogo sana lengo nataka tutengeneze makataba ndogo 100 katika vijiji 100 na kila maktaba itakuwa na vitabu 100...hapa sasa hivi tunafanya maongezi na jamaa wa sola, tukifanikiwa kwasababu na wao watakuwa wanatangaza bidhaa zao wanaweka sola pale kwa ajili ya vijiji ambavyo viko ndani kabisa" ameendelea kusema Nikki ambae ni msemaji mkuu wa Weusi.

Kwanini shilingi mia na si zaidi na nini umuhimu wa kushiriki katika kampeni hii?

Ni shilingi mia kwasababu tunataka hata watu wa chini wa-take action  katika kusapoti elimu na kuleta changes, kwasababu tumezoe kuona NGO mpaka  msaada utoke ulaya au watu wa ulaya au sio au watoe msaada watu wakubwa wenye uwezo lakini hata sisi watu wa kipato cha chini tunaweza kuleta mabadiliko katika jamii.......


No comments:

Post a Comment

paulmkale