Picha,Yemi Alade akishoot video ya ngoma yake mpya‘Taking Over Me’

Ukiangalia video yake ya ‘Johnny’ na ‘Tangarine’, au namna alivyofanya vizuri kwenye video ya ‘Baby Hello’ ya staa mwenzake wa Nigeria, Wande Coal; unaona ni jinsi gani staa huyu wa muziki Yemi Alade yuko vizuri kwenye kuifanya video kupendeza.

Ana nyimbo kali kibao, collabo pia ambazo zimefanya Afrika tumtambue staa huyu kutoka Nigeria, mpya kutoka kwake ni kwamba ametupa ishara tukae tayari kuiona video yake mpya muda wowote kuanzia sasa.

Kashea na sisi picha za Behind the Scenes, wimbo ulifanywa na Producer GospelonDeBeatz, wimbo unaitwa ‘Taking Over Me’ humo ndani kapewa collabo staa mwingine kutoa Naija, rapper Phyno.

Kingine ni kwamba video hii inafanywa Nigeria na South Africa, nimeshea na wewe hizi za Behing the Scenes.

No comments:

Post a Comment

paulmkale