Ommy Dimpoz aelezea sababu za kuzuiwa uwanja wa ndege Marekani na kurudishwa Bongo

Ommy Dimpoz mzee wa "Tupogo" , weekend iliyopita alizuiwa uwanja wa ndege wa Marekani na kurudishwa Tanzania na ndege iliyofata na hivyo kumsababishia kushindwa kufanya show aliyotegemewa kuifanya siku ya jumapili ya tarehe 16, Lasvegas.kwa mujibu wa habari zilizokuwa zimeenea na zilizotoka katoka chanzo cha karibu , zilikuwa zinadai kuwa Ommy karudishwa sababu visa aliyokuwa nayo ilikuwa  ni visa isimruhusu kufanya show Marekani bali ilikuwa ni visa ya kwenda kutembea. Leo hii tumeongea  na Ommy ambae amerejea siku ya Jana

"kilichotokea ni kwamba mimi nilitoka hapa nikaenda mpaka Amsterdam na Amsterdam nilikuwa na connect flight kutoka Amsterdam kwenda detroit na detroit kwenda Vegas kwahiyo kufika Amsterdam nilimiss flight ya connect Amsterdam kwenda detroit kwa hiyo ikabidi ni rebook booking yangu ili nipate flight nyingine ya kwenda Las Vegas kwa hiyo nikakosa connection ya kwenda detroit nikapata connection nyingine ya kupitia Minnesota nilivyofika kule wakati nimefika airport ndege ambayo nilipata connection na hii ya pili ikawa tayari ilikuwa imenichelewesha kwasababu ilikuwa inatakiwa inifikishe siku ya show  sasa  pale kukawa na tatizo kule watu wa venue siku ambayo waliokuwa wameongea nao" amesema Ommy Dimpoz


"kwa hiyo ikabidi waongee kuwa msanii amechelewa lakini tunaomba event tufanye siku nyingine lakini wale jamaa wakakataa wakasema haiwezekani na lengo ilikuwa mimi ni perform kwenye hiyo weekend ya rugby kwa hiyo kutokana na mazingira hayo ikabidi wale watu wa immigration unajua siku zote ukifika ile ni nchi unavyoingia siku zote lazima kuna maswali ya security pale lazima uulizwe, unajua watu hawajui kitu kimoja kwamba kupata visa sio ndio kuingia kwenye nchi ya mtu kwamba ukifika nchi yoyote hata sisi tunaenda South Africa naona ni nchi ambayo tunaingia bila visa ukifika airport lazima uulizwe unakuja kufanya nini, unakaa siku ngapi, kwa hiyo nchi zote utaratibu ndio huo kwa hiyo katika pale kuulizwa nikawambia naenda Las Vegas kwenye show,kwahiyo wakapiga simu kule kwa  watu wa event pamoja na sehemu ya  Venue kwa hiyo watu wa Venue wakaambiwa kulitakiwa kuwe na show ila msanii hakufika kwa hiyo wakabidi waongee na promote akasema tumeisongeza kwasababu msanii amechelewa amemiss flight sasa wakarudi kwangu wakaniambia lengo lilikuwa uje kwenye hii show na show tayari umeshaimiss kwasababu ya matatizo ambayo sisi hatutakiwa kuyajua yamesababishwa na nini  wakasema kwamba lakini hapa inaonesha una show nyingine New york tarehe 21 nikawaambia ndio nilikuwa ninayo ila nilipanga nikitoka Las Vegas naelekea huko" aliendelea kusema


"Wakaniambia sasa hii show ndio tunatatizo nayo kwasababu ni show ambayo inahusisha chama cha kisiasa na kama uliona hata kwenye promotion  yangu nilikuwa nimeandika kuwa nitakuwa na show ya miaka 38 ya CCM Marekani, unajua vyama cha siasa hivi Chadema, CCM wanamatawi yao kule Marekani watu wanaoishi nje mara nyingi uwa wanafanya sherehe sherehe za Annivesary , kwa hiyo wakaniambia kuwa hii visa yako haikuruhusu wewe kuperform kuna aina ya Visa ya inayoruhusu msanii ku perform kwasababu show yako ni kama ya kisiasa, kwa hiyo kwa kuangalia hivyo wakaniambia option iliyopo itabidi nirudi nyumbani  kwasababu shughuli iliyokuleta imeshindikana kwa hiyo unaweza ukaja mwenyewe baadae kwa matembezi yako au kwa nini lakini hata ikitokea mfano leo nikakatiwa ticket au nikate ticket nirudi Marekani visa yangu sasa hivi hainiruhusu kwa hiyo ina maana ninataka kuchukue visa nyingine yenye kibali maalumu chenye kuperform mimi kwenye show."


No comments:

Post a Comment

paulmkale