Tuzo za watu zaja kivingine, vipengele vyaongezeka

Mtu wangu wa nguvu ninayo furaha kushare na wewe stori hii ya hizi tuzo zingine za kutoka Tanzania ambazo hizi zipo kwa ajili ya wale wanaofanya vizuri kwenye sekta mbalimbali.

Nimeambiwa kwamba kuna vipengele vipya viomeongezwa ambavyo mwaka jana havikuwepo,vimeongezwa vipengele 3,kama unakumbuka mwaka jana vilikuwa 11.

Vipengele vilivyoongezwa ni Muongozaji wa filamu anayependwa,tovuti/blogu inayopendwa na mfadhiri maarufu ambaye anapendwa.

Taarifa ikufikie mtu wangu kuwa zoezi la kupendekeza majina ya washiriki limeanza leo kupitia tovuti ya www.tuzozetu.com au unaweza kuandika sms neon TZW code ya hicho kipengele na jina la anayependekezwa kwenda 15678.

Kama uko kwenye mitandao ya kijamii wanayo Hashtag yao ambayo unaweza kuitumia mtu wangu ambazo ni #TZW2015 na #TuzozaWatu.

No comments:

Post a Comment

paulmkale