Diamond amefunguka kuwa hana bifu na msanii mwenzie Ali Kiba..

Akizungumza katika kipindi cha XXL japo Diamond alionyesha kutotaka kulizungumzia hili alisema:
"Sijawahi kuwa na beef nae hata siku moja na tuko poa"
Kuhusu kuwepo kwa hizi team diamond na Team Kiba,  diamond amesema:
"wakati mwingine ni vitu vinakuwa vinatokea katika kazi ambayo kwa mtazamo wangu mimi sioni ubaya wowote, unajua kila mtu ana maamuzi ya kumshabikia mtu anayemtaka yeye, huwezi kumforce mtu awe yanga unakuwa unamlazimisha, ni vitu kama hivyo, so sidhani kama kuna ubaya wowote, kwa baadhi ya watu wakiamua kuutumia kiubaya ndo watakuwa wanakosea, kwa mtazamo wangu naamini panapokuwa na changamoto ndo panafanya muziki wetu ukue, unakuwa mkubwa lakini sasa ifikie time kama mashabiki, mimi kwa akili yangu ndogo ninavyohisi wachukue msanii flani wawashindanishe na wasanii wa nje, kwa sababu ukishindanisha wasanii wa Tanzania kwa Tanzania haiwezi kuleta impact yoyote katika industry yetu, mimi nikabidhi davido, flani mkabidhi wizkid, kila mtu akapige ushindi halafu alete nyumbani."

No comments:

Post a Comment

paulmkale