UFALME
umeanguka! Unaweza kusema hivyo! Hatimaye Miss Tanzania 2006, aliye pia
staa wa filamu za Bongo, Wema Isaac Sepetu amedaiwa kutimuliwa kwenye
nyumba ambayo alipanga kwa mbwembwe na kualika waandishi wa habari ili
watoe ‘nyuzi’ hewani, akidai ni yake kwa kuinunua kwa shilingi milioni
280, fuatana na Ijumaa Wikienda. Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Wema
amekumbwa na kadhia hiyo ya kuhamishwa kwenye nyumba hiyo iliyopo
Makumbusho jijini Dar, usiku wa Desemba 18, mwaka huu.
SIKIA CHANZO
“Jamani
mmesikia kilichomtokea Wema Sepetu? Yaani huyu dada anaishi kwa maigizo
hadi basi. Lile sakata lake la kudaiwa kutumia umeme na maji
kimagumashi limemtokea puani, maana kwenye umeme pekee yake nasikia
anadaiwa zaidi ya shilingi milioni nane (8,000,000) fedha ambazo imekuwa
shida kulipa.”
BABA MWENYE NYUMBA
AINGIA KATI “Sasa baba mwenye
nyumba ameingilia kati. Ameamua kulipa yeye deni hilo lakini akamtaka
Wema ahame haraka kwenye nyumba yake,” kilisema chanzo.
SIKU
YA TUKIO Paparazi wetu alizidi kupenyezewa ‘ubuyu’ kuwa, muda huo tayari
kuna lori aina ya Toyota Canter linahamisha vitu nyumbani kwa Wema na
kwamba, kuna kila dalili anahama baada
ya baba mwenye nyumba wake kumtimua.
PAPARAZI NYUMBANI KWA WEMA
Ilibidi
paparazi wetu akimbie kwa pikipiki iendayo kasi mpaka nyumbani hapo na
kukuta kweli lori likibeba vitu mbalimbali huku wabebaji wakitokwa jasho
chapachapa. Gari hilo lilisimama kwenye lango kuu la kuingilia ndani ya
nyumba hiyo huku likiwa na shehena ya mafurushi ya mizigo. Wakati
paparazi wetu akiwa kwenye hali ya mshangao, aliendelea kuona mizigo
mbalimbali ikitoka ndani ya mjengo huo huku vyombo anuai vya ndani, kama
kabati na baadhi ya makochi yakiwa nje ya nyumba hiyo yakisubiri
kupakiwa tayari kwa safari ya kumuondoa Wema kwenye mjengo huo.
WEMA HAYUPO
Swali la kwanza kwa wabebaji hao kutoka kwa paparazi wetu ni wapi alipo Wema. “Unamtaka Wema wa nini wakati
unajua hayupo hapa, kwanza wewe nani?” alikuja juu mpakiaji mmoja.
PAPARAZI ANUSURIKA KIPIGO
Katika
hatua nyingine isiyokuwa ya kawaida, wapakiaji wengine walitaka
kumshushia kipigo paparazi wetu baada ya kuona mwanga wa kamera wakati
akichukua picha kadhaa kwa ajili ya ushahidi. WALIKOHAMIA Uchunguzi wa
awali, Wema amehamia Mbezi Beach, Dar. Hata hivyo, tangu sakata la wizi
wa maji na umeme, Wema hajawahi kulala na kuamka ndani ya nyumba hiyo
huku habari zikisema amekuwa akiishi mahotelini kama ‘digidigi’.
KWA
NINI WEMA ALISEMA NYUMBA NI YAKE? “Kuna watu wengi walikuwa hawatambui
kwa nini Wema awali alisema hii nyumba ni yake. Mwanzo wakati anahamia,
pia alikuwa ana mazungumzo na baba mwenye nyumba kwamba ainunue lakini
watoto wakagoma hivyo Wema akawa analipa kodi kila mwaka.
WEMA,
PETIT MAN Juzi, Wema hakupatikana hewani ili kujibu madai hayo, lakini
mmoja wa watu wake wa karibu, Petit Man alikumbana na paparazi wetu
katika klabu moja jijini Dar, alipoulizwa kuhusu mambo hayo alikiri Wema
kuhama kwenye nyumba hiyo. “Tena sasa tunahamia kwenye nyumba
aliyonunua Wema mwenyewe. Bonge la nyumba, mtaipata habari yake. Iko
Mbezi Beachn alisema Petit.
No comments:
Post a Comment
paulmkale