Diamond Atoa Nafasi Kwa Video Queen wa Kike Toka Bongo Kwenye Video Mpya Aliyofanya na Raymond Kama Upo Tayari Maelezo Yako HAPA


Baada ya kupigiwa kelele sana kuhusu kutumia wanawake wa kizungu kwenye video zake, Diamond amelegeza moyo wake na sasa ameamua kuwapa nafasi warembo wa Bongo. 
Staa huyo ametangaza kuwa wiki hii ataanza kushoot video ya wimbo aliomshirikisha msanii aliyechini ya label yake ya WCB, Raymond na kuwataka wasichana wote wanaodhani wana urembo wa kuing’arisha video yake wazeme kwenye DM.
“Shooting my other HIT ft Ray Vanny next week in Dar / Tanzania. If you are cute & African Queen and you would love to be part of it DM me,” alitweet mwishoni mwa wiki.
Alidai kuwa video hiyo itakuwa na maudhi ya Kiafrika. Hata hivyo haijajulikana iwapo atatumia muongozaji wa nyumbani ama atamdondosha muongozaji wa Afrika Kusini.
Aliwahi kumleta God Father kushoot sehemu ya video ya wimbo wake ‘Utanipenda’ pamoja na video ya Raymond, Kwetu.
Hata hivyo kwa sasa ameonekana kupenda kufanya kazi na Nick aliyeongoza video ya Bado, Make Me Sing na Ibaki Story.

No comments:

Post a Comment

paulmkale