Baada tu ya kutoka kurekodi collabo ya Coke Studio ZA na Cassper
Nyovest, Diamond Platnumz aliingia location kushoot video ya wimbo
alioshirikishwa na staa wa Zimbabwe, Jah Prayzah.
Prayzah ambaye jina lake halisi ni Mukudzei Mukombe alilazimika
kusafiri hadi Dar es Salaam kuja kukamilisha collabo yake na Diamond
hivi karibuni.
Jah Prayzah ambaye hujulikana pia kwa jina la Musoja kutokana na
kupenda kuvaa nguo za kijeshi, amemshirikisha Diamond kwenye wimbo wake
uitwao Watora Mari.
Wimbo huo utapatikana kwenye album yake mpya na ya saba, iitwayo Mudhara Vachauya itakayozinduliwa August 12.
Diamond ameshare picha Instagram akiwa na staa huyo na kuandika:
Wraping it up my Zimbabwean brother @jahprayzah Video #Kidogo before
spending time with my Miss world!”Jah Prayzah naye ameshare video akiwa na Diamond kuelezea ujio wa video yao.
No comments:
Post a Comment
paulmkale