Wanaotaka kumnunua Messi waambiwa hivi.
Mshindi wa tuzo ya Mchezaji bora wa dunia mara nne Lionel Messi
hataihama klabu yake ya Barcelona kama ilivyoanza uvumishwa kwenye baada
ya magazeti barani ulaya baada ya kuthibitisha kuwa ataendelea kubaki
na klabu yake ya Barcelona kwa muda mrefu zaidi.
Kwa mujibu wa gazeti la michezo nchini Hispania la Mundo Deportivo,
Messi ambaye ni nahodha wa pili wa Barcelona hataihama klabu hiyo na
badala yake ataendelea kucheza hapo kwa miaka mingi zaidi kwa klabu hiyo
ni kama nyumbani kwake .
Tayari matajiri wa kiarabu na kirusi wanaomiliki klabu za Paris St
Germain na Chelsea walishaanza mipango ya chini chini ya kumsajili nyota
huyo kwenye klabu zao baada ya kufahamishwa kuwepo kwa hali ya
kutoridhika kwa nyota huyo ndani ya klabu yake .
Tajiri wa Chelsea Roman Abramovich alikuwa anafanya mpango ambapo
alikmhusisha nyota wa zamani wa Barcelona Cesc Fabregas ambaye ni rafiki
wa karibu wa Messi akimtaka nyota huyo Mhispania kusaidia kumsaidia
kumshawishi Messi kuhamia London .
Katika mpango huo pia alihusishwa mpenzi wa Fabregas Daniella Seeman
ambaye ana ukaribu na mpenzi wa Messi na katika majaribio yote hayo
hakuna aliyeweza kufanikiwa kuwa na ushawishi wa nguvu kwa Messi.
Nasser AL-Khelaifi ambaye ni tajiri wa klabu ya PSG ya nchini
Ufaransa akiiwakilisha familia ya kifalme ya nchini Qatar ambao ndio
wanaimiliki klabu hiyo bingwa ya Ufaransa naye alikuwa anaandaa ofa ya
kumnunua Messi kwa kiwango chochote kile cha fedha ambacho Barcelona
wangetaka endapo wangekuwa tayari kumuuza .
Messi ameichezea Barcelona tangu akiwa na umri wa miaka 13 na amekuwa
wazi kutamka kuwa Barcelona ndio klabu pekee ambayo ataichezea maisha
yake yote akiwa ulaya .
Hivi karibuni kumekuwa na tetesi nyingi kuhusiana na nyota huyo kuwa
na maisha yasiyo na raha ndani ya Barcelona hali ambayo hata hivyo
uongozi wa klabu hiyo umekuwa mstari wa mbele kukanusha .
No comments:
Post a Comment
paulmkale