Watu Wa Africa Magharibi Wazuiwa Kuingia Kweye Nchi Hii

Stop Ebola

Serikali ya Australia imetengaza kuzuia kuingia mtu yoyote anayetokea nchi za Afrika Magharibi zilizoathiriwa na Ebola, Guinea, Liberia na Sierra Leone kama njia ya kujikinga na hatari ya kuingia kwa ugonjwa huo nchini humo.

Mbali na taarifa iliyotolewa na chama cha madaktari Australia (AMA) iliyosema kuwa nchi hiyo haiko kwenye hatari ya kupatwa na maambukizi ya virusi vya ugonjwa huo, waziri wa uhamiaji Scott Morrison ametangaza utaratibu ‘mgumu’ kwa mtu yoyote anayetoka Afrika Magharibi kuingia nchini humo.

Akiongea katika bunge la nchi hiyo, Morrison amesema kwa sasa wanasitisha maombi yote ya vibali vya kuingia nchi hiyo kwa mtu yoyote anayetokea Afrika Magharibi, na kwa yeyote mwenye hati ya kudumu ya kuingia nchini humo, unaandaliwa utaratibu wa kuwapo sheria itakayowalazimu kukaa karantini ndani ya nchi wanakotoka kwa takribani wiki 3 kabla ya kuanza safari ya kwenda Australia.

Kwa upandee wake waziri mkuu wa Australia, Tony Abbott amesema hakubaliani na taarifa ya chama cha madaktari inayosema Australia haiko katika hatari ya kupata maambukizi ya Ebola, na kukosoa kuwa taarifa hiyo haijazingatia maslahi ya taifa hilo.

Baadhi ya wabunge wa upinzani wamekosoa maamuzi ya serikali ya nchi hiyo kwa kusema kitendo cha kuzuia watu wanaotokea Guinea, Liberia na Senegal wasiingie nchini humo hakioneshi picha nzuri ya taifa hilo.

No comments:

Post a Comment

paulmkale