Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2015(KTMA) iko tayari soma hapo.

Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa kushirikiana na Kilimanjaro Premium Lager wamezindua rasmi msimu mwingine wa tuzo za muziki Tanzania unaojulikana kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards (KTMA).

Meneja wa bia ya Kilimanjaro Pamela Kikuli amesema; “Kilimanjaro Premium Lager ni bia ya watanzania na imejikita katika kuwaletea burudani na pia kutoa majukwaa ambayo yanawapa Watanzania fursa ya kukuza vipaji mbalimbali.. hii tumeithibitisha kwa juhudi za makusudi za kutenga fungu kubwa na kuongeza ushiriki wa wataalaam mbali mbali kwenye fani husika ili kuziendeleza, kuzikuza na kuziongezea thamani tuzo hizi mwaka hadi mwaka sambamba na umaarufu kuongezeka kwenye medani za Kimataifa.”

Kampuni hiyo imewekeza zaidi ya Tshs. Bil.1 kuhakikisha ubora wa hali ya juu unajitokeza kwenye mchakato mzima wa tuzo hizi.

Msimu huu hauna mabadiliko makubwa sana katika vipengele wala mfumo wa kuwapata wasanii watakaoshiriki, kuna maboresha kwenye njia za upigaji kura kwa mfano kwa sasa ni watu wengi wanatumia Whatsapp, KTMA imewarahisishia kwa kuongeza njia hiyo kwenye mchakato wa kupendekeza na kupiga kura.

Kura za maoni zitaanza kupigwa tarehe March 30 ambapo shabiki ataweza kupendekeza nani ama nyimbo zipi ziwemo kwenye vipengele vyote vya KTMA 2015.

Watu watapiga kura kupitia mtandao, Whatsapp na SMS na utaratibu uliopo ni kwamba namba moja ya simu itatumika kupiga kura moja kwenye kila kipengele.

Hizi ni njia ambazo utazitumia kupiga kura;

  1. Whatsapp – 0686 528 813.

  2. SMS – 15415.

  3. Mtandao – www.ktma.co.tz

BASATA wamesisitiza usimamizi mzuri wa nyimbo zinazoingizwa; “Kama kuna wimbo ulifungiwa na BASATA hautaruhusiwa kushiriki kwenye mchakato“– BASATA.

No comments:

Post a Comment

paulmkale