New Music: Nikki Mbishi,One,Songa & Pro7- Tukutane Kilingeni/Download
Nyimbo nyingine mpya ya Nikki Mbishi iitwayo TUKUTANE KILINGENI humu akiwashirikisha wan Hiphop wenzie kutoka Lunduno Songa, One Incredible na Pro.7 na mtayarishaji akiwa ni Invisible KTB.
Ni time yako sasa kuisikiliza na Kuidownload pia...!!!
New Music: 20% - Atoe/Download
Msanii aliyewahi kushinda tuzo Tano za Tanzania Kili Music Awards Twenty Percent arudi upya na Nyimbo mpya iliyoandaliwa na Production nyingine kabisa ambayo Twenty hakuwahi kufanya Ngoma katika Studio hiyo. Nyimbo aliyoifanya inaitwa ATOE huku ukwa na ujumbe mzito ndani yake, wimbo huu umetayarishwa na(Produced by) Dizzy chini ya studio ya Pure Records iliyopo Moro Town.
Ni time yako sasa kuusikiliza na Kuudownload pia...!!!
Tulizipokea taarifa za kifo cha Abdul Bonge wa Tiptop Connection ila hiki ndio chanzo cha kifo
Saa zinahesabika toka Tanzania na familia ya bongofleva ipokee taarifa za msiba wa Abdul Bonge Mwanzilishi wa kundi maarufu la Bongofleva Tiptop Connection lenye wanachama kama Tunda Man, Madee, Dogo Janja na wengine waliopita kama Keisha, Cassim Mnganga na MB Dogg.
Jioni ya March 28 2015 ndio taarifa zilianza kusambaa lakini chanzo cha kifo cha ghafla cha Abdul hakikuwa kimesemwa lakini mdogo wake ambae ni Babu Tale ameongea na AyoTV na kusema >>> ‘Kuna mshkaji wetu mmoja alikua anagombana na mke wake jirani yetu, wakamfata hapa Abdul aende… mara ya kwanza na ya pili akakataa, mara ya tatu akasema ngoja aende’‘Alivyoenda ukapita ukimya kidogo, baadae kuna mtu akaja kumuita kaka yetu mkubwa mwingine na kumwambia nenda kamsaidie kaka yako mkubwa amedondoka, kaka yangu baadae akanipigia simu akasema Bonge kama amezimia lakini sidhani kama atapona sababu wakati wa kuamulia ugomvi alianguka baada ya kusukumwa nafikiria aliangukia kichogo, kumpeleka Hospitali Manzese wakasema ameshafariki‘ – Babu Tale.
R.I.P Abdul Bonge |
Bab Tale ameongea kwa hisia sana na kuizungumzia pia familia yao.
Taarifa kutoka msibani leo March 29 2015 zinasema Abdul atasafirishwa kwenda kuzikwa Morogoro baada ya mwili kuzuiliwa leo mpaka uchunguzi ukamilike, kwa sasa Watu mbalimbali wakiwemo wasanii wa bongofleva wako Tiptop Manzese kwenye kutoa pole, mwili unatarajiwa kusafirishwa kesho kwenda Morogoro.
Naambiwa maziko yatafanyika kijiji cha Mkuyuni Morogoro, kwa asiyepajua Mkuyuni ni njia ya kwenda Matombo. #RIP #AbduBonge
New Music: Chege & Temba ft Ommy Dimpoz - Nikiss Nikukiss/Download
Sikiliza hapa na download ngoma mpya kutoka kwa Chege na Temba"NIKISS NIKU KISS"Wakiwa na mkali wa Tupogo Ommy Dimpoz.
New Video: Tammy – Down Low (Official Music Video)
Bang Bang Music & Entertainment Company Presents Tanziania Finest
Female Mcee Tammy A.K.A The Baddest With Her 2nd Music Video Produced By
Pancho Latino From BHITS And Directed By JoowzeyTz From BangFILMs.
New Video: Team Racers - TRLG Tunavuka Mipaka (Official Music Video)
Hip Hop / Trap Song Preformed By TEAM RACERS Audio Produced By DQ Video Directed, Shot And Edited By GQ Digital Vibes + Lion Head Production +255 656650688 KACCI Team Spokesman
New Music: Bell 9 - Shauri Zao/Download
Ni time yako sasa kupakua kile kitu kpya kutoka kwa Bell 9"SHAURI ZAO"Kilichofannyikia pale kili Records,Bofya hapo kusikiliza na kudownload mtu wangu.
New Video: Diamond Platnumz ft Khadija Kopa - Nasema Nawe(Official Music Video )
Diamond Platinumz anakuletea video ya ngoma yake mpya"NASEMA NAWE"Akiwa na Khadija Kopa Mwimbaji wa taraabu.‘Nitampata Wapi‘ ni hit ya mkali anayeiwakilisha vizuri TZ kupitia muziki anaoufanya, Diamond Platnumz.. Jina lake sio geni kwa wapenzi wa muziki Afrika. Ngoma hiyo aliyoitoa mara ya mwisho bado inafanya vizuri.. Wanigeria wanatoa ngoma mpya kila siku, Diamond nae anataka kuwa kama wao?bofya hapo kuitazama sasa..
New Video: Barnaba - Suna (Official Music Video)
Barnaba anakuletea video ya wimbo wake mpya"SUNA"ikiwa imetayarishwa na(Produced by) *C9 Kanjenje* na video kuongozwa na (Directed by) *Nick Dizo* wa Focus Film.Bofya hapo kuitazama..
AFYA YA MAMA DIAMOND, TUMUOMBEENI!
TUMUOMBEE! Afya ya mama mzazi wa msanii nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumz, Sanura Kassim ‘Sandra’ bado si shwari juzikati hali yake ilibadilika ghafla na kuilazimu familia yake kumkimbiza katika Hospitali ya TMJ iliyoko Mikocheni jijini Dar ambako amepewa kitanda, Ijumaa limetonywa.
Chanzo cha uhakika kililieleza gazeti hili kuwa mama Diamond ambaye amekuwa akisumbuliwa na maradhi yenye kuashiria kupooza, juzikati alizidiwa na kusababisha ndugu zake wampeleke hospitali.
“Mamake Diamond ana wiki sasa hospitalini, lakini mwenyewe Diamond hataki watu wajue, anakwenda kwa kujificha, wakati mwingine hadi saa saba usiku, sijui anaficha nini wakati suala lipo wazi tu, nadhani tukeshe tukimuombea ili hali yake iweze kurudi kama zamani,” kilisema chanzo chetu.
Gazeti hili lilifunga safari hadi hospitalini hapo ili kujiridhisha juu ya habari hizo, lakini mhudumu mmoja aliyeulizwa juu ya uwepo wa mama huyo, alikubali kuwa ni kweli amelazwa hapo, lakini lisingeweza kuruhusiwa kumuona bila ruhusa ya Diamond au wanafamilia.
Diamond alipotafutwa kuzungumzia afya ya mama yake aligoma kusema lolote zaidi ya kuomba aachwe kwani wanao uwezo wa kuzungumzia mambo mengine bila kugusia kuhusu mzazi wake.“Naomba unipe muda maana nina matatizo sana, hata kuzungumzia ishu hiyo nadhani hakuna haja,” alisema Diamond.
New Video: Chaba - Haijatosha.(Official Music Video)
Music video by Chaba performing "Haijatosha" (Ft.Daz Naledge & Wise
Man). (C) 2015 Red Films Tanzania/Dab Muzik/Watengwa Recs.Inc
New Video: Vanessa Mdee ft. K.O - Nobody But Me(Official Music Video)
Sifa nyiiiingi zipo pia kwa V Money a.k.a Vanessa Mdee ambae ni mkali wa bongofleva kwenye hits kama ‘come over’ ‘closer’ ‘safari’ na nyingine ambazo zimemfanya awepo bongoflevani na sasa katuletea hii mpya kafanya na rapper K.O wa South Africa.
New Music: Vanessa Mdee feat K.O - Nobody But Me/Download
Ni time yako sasa kupakua hapa wimbo mpya wa VANESSA MDEE aliomshirikisha msanii K.O kutoka Afrika ya Kusini, wimbo unaitwa "NOBODY BUT ME"
Tuzo za watu zaja kivingine, vipengele vyaongezeka
Mtu wangu wa nguvu ninayo furaha kushare na wewe stori hii ya hizi tuzo zingine za kutoka Tanzania ambazo hizi zipo kwa ajili ya wale wanaofanya vizuri kwenye sekta mbalimbali.
Nimeambiwa kwamba kuna vipengele vipya viomeongezwa ambavyo mwaka jana havikuwepo,vimeongezwa vipengele 3,kama unakumbuka mwaka jana vilikuwa 11.
Vipengele vilivyoongezwa ni Muongozaji wa filamu anayependwa,tovuti/blogu inayopendwa na mfadhiri maarufu ambaye anapendwa.
Taarifa ikufikie mtu wangu kuwa zoezi la kupendekeza majina ya washiriki limeanza leo kupitia tovuti ya www.tuzozetu.com au unaweza kuandika sms neon TZW code ya hicho kipengele na jina la anayependekezwa kwenda 15678.
Kama uko kwenye mitandao ya kijamii wanayo Hashtag yao ambayo unaweza kuitumia mtu wangu ambazo ni #TZW2015 na #TuzozaWatu.
Iyanya feat Diamond Platinumz - (I love)Nakupenda BTS
Tazama hapa iyanya akiwa anaiianda video ya ngoma yake mpya"I LOVE"Ambayo yuko na msani kutoka TZ Diamond Platinumz.
New Video: Shetta Ft. K Cee - Shikorobo (Official Music Video)
Ni zamu ya Shetta ambae ni mkali wa bongofleva aliekaa kimya bila kutoa chochote kipya kwa zaidi ya miezi 7 na sasa amerudi kwenye headlines na hii kolabo kampa shavu Kcee wa Nigeria.Tazama hapa video hii kali iliyofanyika Africa Kusi na Dir-GoodFather.
New Video:DJ Xclusive feat. Banky W & Niyola - Tonight (Official Video)
EME is proud to present "Tonight" the banging new video featuring
Superstar Dj Xclusive, Banky W & Niyola. The video was directed by
Banky W & Adasa... and written & produced by Banky W once again.
The song was produced by hitmaker extraordinaire Masterkraft, features
DJ Xclusive on the intro & outro, a solid vocal performance by
Niyola, as well as Banky W multitasking by singing and rapping. The
story line is a hilarious take on guys that spend a lot of money in the
club, and expect something in return from the women they spend it on.
Shot in Lagos at Club Quilox, "Tonight" features appearances from many
stars including CDQ, Shaydee, Big Mo, Uzzy Tebudiga, DNMT, and last but
not least, a hilarious cameo of Banky once again appearing as Aristo W
(of "Jasi" fame). We hope you enjoy watching this as much as we enjoyed
filming it.
New Music: Shetta feat K Cee - Shikorobo/Download
Shetta anakuletea ngoma yake mpya"SHIKOROBO"Aliyomshilikisha msani maarufu kutoka Nchini Nigeria K Cee,Bofya hapo kusikiliza na kudownload ngoma hii iliyotayarishwa na Prod-Tudd Thomas.
Kaa Tayari; Bell 9 kuja na hii"SHAURIYAO"ijuma hii
Muimbaji kutoka mji kasoro bahari Morogoro Bell 9anatarajia kudondosha mzigo mpya ukwendao kwa jina la "SHAURI YAO"Bell 9 amesema ngoma hii itakuwa hewan rasmi ijumaa hii ya Tar-27 March 2015.Ngoma hiyo imefanywa na Prod Rush Don pale Kiri Records.Kuhusu mipango ya video Bell amesema inategemea ngoma itapokelewa vipi,Lakini alisema upo uwezekano wa kufanya video kwenye wimbo mwingine maana ninanyimbo nyingi alisema Bell 9.
Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2015(KTMA) iko tayari soma hapo.
Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa kushirikiana na Kilimanjaro Premium Lager wamezindua rasmi msimu mwingine wa tuzo za muziki Tanzania unaojulikana kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards (KTMA).
Meneja wa bia ya Kilimanjaro Pamela Kikuli amesema; “Kilimanjaro Premium Lager ni bia ya watanzania na imejikita katika kuwaletea burudani na pia kutoa majukwaa ambayo yanawapa Watanzania fursa ya kukuza vipaji mbalimbali.. hii tumeithibitisha kwa juhudi za makusudi za kutenga fungu kubwa na kuongeza ushiriki wa wataalaam mbali mbali kwenye fani husika ili kuziendeleza, kuzikuza na kuziongezea thamani tuzo hizi mwaka hadi mwaka sambamba na umaarufu kuongezeka kwenye medani za Kimataifa.”
Kampuni hiyo imewekeza zaidi ya Tshs. Bil.1 kuhakikisha ubora wa hali ya juu unajitokeza kwenye mchakato mzima wa tuzo hizi.
Msimu huu hauna mabadiliko makubwa sana katika vipengele wala mfumo wa kuwapata wasanii watakaoshiriki, kuna maboresha kwenye njia za upigaji kura kwa mfano kwa sasa ni watu wengi wanatumia Whatsapp, KTMA imewarahisishia kwa kuongeza njia hiyo kwenye mchakato wa kupendekeza na kupiga kura.
Kura za maoni zitaanza kupigwa tarehe March 30 ambapo shabiki ataweza kupendekeza nani ama nyimbo zipi ziwemo kwenye vipengele vyote vya KTMA 2015.
Watu watapiga kura kupitia mtandao, Whatsapp na SMS na utaratibu uliopo ni kwamba namba moja ya simu itatumika kupiga kura moja kwenye kila kipengele.
Hizi ni njia ambazo utazitumia kupiga kura;
Whatsapp – 0686 528 813.
SMS – 15415.
Mtandao – www.ktma.co.tz
BASATA wamesisitiza usimamizi mzuri wa nyimbo zinazoingizwa; “Kama kuna wimbo ulifungiwa na BASATA hautaruhusiwa kushiriki kwenye mchakato“– BASATA.
Jose Chameleone kuingia kwenye Coce Studio Africa Mwaka huu
Msimu mpya wa Coce Studio Africa maandalizi yameshaanza rasmi,Vyombo vya habari vimedai kuwa Dr Jose anaweza kuwa ni mmoja wa washiliki kutoka nchini Uganda.Chameleone ataungana na masta mbalimbali kutoka afrika katika show hiyo ikiwa na msimu wa tatu.Tanzania mwaka jana walioshiliki ni Vanessa Mdee,Diamond Platinumz,Joh Makini,Shaa.Inasemekana mwaka huu Ali Kiba nae atakua ni mmoja ya watakaoingia kwenye show hiyo.
New Music: Sura One Feat Menina - Tuli Tuli/Download
Sura One anakuletea ngoma yake mpya "TULI TULI"Aliyomshilikisha mwanadada Menina,Bofya hapo kusikiliza na kudownload kichupa hiki kilichotayarishwa na Pro-Maneke.
NUH MZIWANDA atakuwepo TANGA Jumamosi hii ya tarehe 28.3.15
Tanga Tanga kaa tayari kwa @mziwandanation na team yake nzima ya kazi ndani ya lacassa chica jumamosi hii #BilimaTour. Mlangoni shilingi 10000, ukikata tiketi mapema shiling 7000
Zari The Boss lady ndani ya nyumba mpya ya Diamond Platnumz.
Zari the boss lady ameshare picha ya chumba cha kulala kwenye jumba la
kifahari la Diamond Platnumz lililopewa jina ‘[State House]. Zari
aliweka picha ya Gypsum ambayo imetengenezwa peke kwaajili ya Diamond
Platnumz huku ujumbe ukisema [Gotta love ny current view]
New Music : Mwaka Mzima Feat. Davizo & Mwiro - Mumyloo/Download
Bofya HAPA https://mkito.com/song/ mumyloo-ft-davizo-mwiro/13649
kupakua wimbo kwa jina "Mumyloo" toka kwa "Mwaka Mzima ft Davizo &
Mwiro ikiwa ni mkono toka Kalizone chini ya Goncher, kwa
mawasiliano/mahojiano zaidi na MWAKA MZIMA check nae kwa nambari +255 755 466 060 powered by @vmgafrica @defxtro @mkitodotcom #SupportYourOwn
New Video: Jason Derulo - Want To Want Me (Official Video)
Tazama hapa video mpya ya Jason Derulo"Want To Want Me"
Jason Derulo's brand new single "Want To Want Me" is available now on iTunes!
Download it here: smarturl.it/WantToWantMe
Download it here: smarturl.it/WantToWantMe
Video Teaser: Shetta Feat. Kcee - Shikorobo
Nakupa sekunde chache kutazama kionjo cha cha video mpya ya Sheta akiwa na K Cee"Shikorobo"video hiyo imefanyika Nchini Afrika Kusini.Inatarajiwa kuachiwa rasmi hapo kesho@paulmkale..
New Music : Galaxy - Tam Tam /Download
Pakua wimbo mpya wa Galaxy #TamTam, msanii chipukizi wa Bongo Fleva.
https://mkito.com/song/tamtam/ 13619
Ngoma mpya ya Shetta akiwa kashirikiana na KCEE 'Shikorobo' kutoka kesho
Kupitia account yake ya Instagram mwimbaji *Shetta* ameeleza namna alivyokuwa anaisubiri kwa hamu siku ya kuachilia ngoma hiyo. Ameandika haya "*Leo ni jumatatu tunashinda kesho Alafu ile jumatano sasa kesho kutwa tarehe 25/3/2015 mzigo huu ambao hata mimi nilikua nasubiri kwa hamu utoke ndio unatoka sasa utapata kusikia na kuona kwa macho yako nikimaanisha Video na Audio kwa pamoja.
Subscribe to:
Posts (Atom)